
John Kerry asema Uganda inakiuka haki za binaadamu
Marekani haikufurahishwa na hatua ya Uganda kuidhinisha sheria dhidi ya wapenzi wa jinsia moja.
Waziri
 wa mashauri ya Kigeni wa Marekani, John Kerry amesema tangu Uganda 
iidhinishe mswada huo miaka minne iliyopita, Marekani ilieleza wazi 
kwamba sheria hiyo inakiuka jukumu la kuhakikisha kuwepo haki za 
binaadamu ambalo tume ya haki za binaadamu Uganda inatambua linaambatana
 na sheria ya Uganda.
Kerry
 amesema,' Baada ya kuidhinishwa sheria hii, tunaanza ukaguzi wa ndani 
wa uhusiano wetu na serikali ya Uganda, kuhakikisha kwamba pande zote za
 uhusiano wetu, ukiwemo miradi ya msaada, zinapinga sera na sheria 
zinazowaonea watu na tuwe na uhusiano unaodhihirisha maadili yetu'.
Tamko 
hilo limetolewa siku moja baada ya rais Yoweri Museveni kukaidi 
shinikizo la kimataifa na kutia saini sheria hiyo iliyo zusha mzozo, 
inayoharamisha mapenzi ya jinsia moja Uganda, hatua iliyozusha hisia 
kali.
Baadhi ya mataifa ya magharibi tayari yanatishia kukatiza msaada wa moja kwa moja kwa serikali ya Uganda.
Marekani
 inasema kuidhinishwa kwa sheria hiyo kunatishia hatari ya kurudi nyuma 
katika uwajibikaji wa Uganda kulinda haki za raia wake na kutishia jamii
 ya wapenzi wa jinsia moja Uganda.Chanzo BBC Swahili
 
No comments:
Post a Comment