
Zanzibar.
 Watu wanne wamejeruhiwa baada ya milipuko minne inayoaminika kuwa ni 
mabomu kutokea katika maeneo matatu tofauti Zanzibar.
Katika 
moja ya matukio hayo, watu wanne walijeruhiwa, mmoja akikatika mguu, 
katika eneo la Unguja Ukuu, Mkoa wa Kaskazini Unguja. Majeruhi wawili 
wamelazwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja, Unguja.
Mkuu wa 
Operesheni wa Polisi, Mkoa wa Kusini Unguja, Hamad Said Masoud alisema 
mlipuko wa kwanza ulitokea juzi katika eneo la Fuaoni Maili Nne wakati 
watu wasiojulikana waliporusha kitu kinachoaminika kuwa ni bomu wakati 
waumini wa Kanisa la Evangelist wakiendelea na ibada ya Jumapili.
Kamishna 
wa Polisi Zanzibar, Hamdan Omar Makame alisema tukio la juzi, kitu 
kinachosadikiwa kuwa ni bomu kilirushwa wakati waumini wa kanisa hilo 
wakiendelea na ibada na kutoa mlipuko na kishindo kikubwa. Alisema 
wakati wakiendelea na uchunguzi wa tukio hilo, milipuko mingine mitatu 
ilitokea jana.
Katika 
mlipuko wa kwanza kwa jana uliotokea saa 6.30 mchana katika kituo kimoja
 cha fundi vyuma aliyetambulika kwa jina la Juma Abdallah huko Unguja 
Ukuu ndiko kulikokuwa na watu waliojeruhiwa.
Waliojeruhiwa katika tukio hilo ni Pandu Haji Pandu aliyekatika mguu na Shaaban Khamis Ibrahim ambaye aliumia sehemu za kiuno.
Hamad alisema mtu mmoja aliokota chuma kizito na kukipeleka kwa fundi akitaka atengenezewe nanga kwa ajili ya uvuvi.
 
No comments:
Post a Comment