Rasimu hiyo ya kanuni inasisitiza kuwa mjumbe 
anayeshindwa kufuata taratibu anawezwa kusimamishwa, na hatapokea posho 
hiyo kwa kipindi chote atakachokuwa benchi.
Hata hivyo, wabunge mbalimbali walisikika leo 
asubuhi wakisema kuwa kiwango hicho cha Sh 220,000 ni kidogo sana, hali 
inayofanya washindwe kumudu gharama za maisha mjini Dodoma.
Richard Ndassa (CCM-Sumve) aliiambia Mwananchi 
kiwango walichowekewa ni sawa na “posho aliyokuwa akilipwa dereva wa 
Tume ya Mabadiliko ya Katiba.” “Hii siyo sawa kabisa,” alisisitiza.
Mbunge wa Kishapu, Suleiman Nchambi alikuwa na 
haya ya kusema: “Sisi tumeshazoea maisha ya Dodoma na tunaishi hivyo 
hivyo tu licha ya kuwa fedha ni ndogo.”
“Ila hawa wenzetu ambao ni wageni hali zao ni mbaya.”
Katika jitihada za kuzima fukuto hilo la posho, 
Mwenyekiti wa muda wa Bunge la Katiba, Pandu Ameir Kificho aliahidi 
kulirudisha suala hilo serikalini ili litazamwe upya. NA MWANAINCHI
 
No comments:
Post a Comment