 Wakati kuna joto la vyombo vya habari vya kimataifa kuituhumu Tanzania
 kuwa haipambani na ujangili, Rais Jakaya Kikwete amesema Serikali 
imeubaini mtandao unaojumuisha watu 40, akiwemo tajiri maarufu mkoani 
Arusha.Akihojiwa juzi jioni na Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Rais Kikwete alikanusha taarifa zilizotolewa na gazeti la Sunday Mail
 la Uingereza zilizodai Tanzania haijafanya juhudi za kupambana na 
ujangili wa meno ya tembo, akisema taarifa hizo ni uzushi na upuuzi 
mtupu.“Gazeti
 hilo limezungumza na nani, ndiyo maana sitaki kupoteza muda kujadili 
upuuzi, achana na mambo hayo. Ndiyo maana tunasema, akutukanaye 
hakuchagulii tusi,” alisema Rais Kikwete.Alisema
 inashangaza kuona watu wanaozusha taarifa hizo hawaoni jinsi 
tulivyofanya jitihada za kutokomeza ujangili, kama operesheni za 
tokomeza ujangili na operesheni kipepeo.Kuhusu
 majangili 40 ambao wametambuliwa, Rais Kikwete alisema wameutambua 
mtandao mkubwa wa majangili unaoongozwa na mfanyabiashara mkubwa wa Arusha Mjini.“Kuna
 majangili 40 waliotambuliwa na tumetambua mtandao mzima, pale Arusha 
kuna mtu mkubwa alikuwa anaendesha biashara. Kazi ilikuwa ni kutambua 
mtandano wote, ule mtandao ni mpana sana,” alisema Rais Kikwete.
Wakati kuna joto la vyombo vya habari vya kimataifa kuituhumu Tanzania
 kuwa haipambani na ujangili, Rais Jakaya Kikwete amesema Serikali 
imeubaini mtandao unaojumuisha watu 40, akiwemo tajiri maarufu mkoani 
Arusha.Akihojiwa juzi jioni na Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Rais Kikwete alikanusha taarifa zilizotolewa na gazeti la Sunday Mail
 la Uingereza zilizodai Tanzania haijafanya juhudi za kupambana na 
ujangili wa meno ya tembo, akisema taarifa hizo ni uzushi na upuuzi 
mtupu.“Gazeti
 hilo limezungumza na nani, ndiyo maana sitaki kupoteza muda kujadili 
upuuzi, achana na mambo hayo. Ndiyo maana tunasema, akutukanaye 
hakuchagulii tusi,” alisema Rais Kikwete.Alisema
 inashangaza kuona watu wanaozusha taarifa hizo hawaoni jinsi 
tulivyofanya jitihada za kutokomeza ujangili, kama operesheni za 
tokomeza ujangili na operesheni kipepeo.Kuhusu
 majangili 40 ambao wametambuliwa, Rais Kikwete alisema wameutambua 
mtandao mkubwa wa majangili unaoongozwa na mfanyabiashara mkubwa wa Arusha Mjini.“Kuna
 majangili 40 waliotambuliwa na tumetambua mtandao mzima, pale Arusha 
kuna mtu mkubwa alikuwa anaendesha biashara. Kazi ilikuwa ni kutambua 
mtandano wote, ule mtandao ni mpana sana,” alisema Rais Kikwete.
Katika
 mahojiano hayo, Rais Kikwete alisema, Tanzania ilikuwa ni nchi yenye 
tembo wengi zaidi duniani, lakini ujangili ulipokithiri, tembo 
walipungua na kufikia 57,000 tu mwaka 1987.
“Mwaka
 1989, Taasisi ya Kimataifa ya Cites, walipiga marufuku biashara ya meno
 ya tembo duniani na ujangili ulipungua kwa kiasi kikubwa hivyo tembo 
waliongezeka na kufikia, 110,000 mwaka 2009,” alisema.
 
No comments:
Post a Comment