 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya 
Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, ameweka wazi utetezi wa Tanzania katika 
mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa na Malawi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya 
Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, ameweka wazi utetezi wa Tanzania katika 
mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa na Malawi.
Akizungumza na wahariri wa habari katika 
semina ya ardhi Dar es Salaam jana, Profesa Tibaijuka alisema tayari 
Rais Jakaya Kikwete ametoa ushahidi wa mpaka huo katika Kamati ya Marais
 Wastaafu, Festus Mogae wa Botswana, Joachim Chisano wa Msumbiji na 
Thabo Mbeki wa Afrika Kusini.
Katika ushahidi huo, kwa mujibu wa Profesa 
Tibaijuka, Tanzania ilitumia zaidi historia ya ugawaji mipaka ilivyokuwa
 na kutumia ushahidi wa nyaraka za serikali za kikoloni, zilizoshiriki 
kugawa mipaka ya Afrika.
Profesa Tibaijuka alisema mipaka ya nchi 
iliwekwa mwaka 1890 katika Mkataba wa Wajerumani waliokuwa wakitawala 
Tanganyika kwa kutumia hadithi za wagunduzi waliotangulia Afrika, kabla 
ya Wakoloni kuanza kugawana bara hilo.
Wakati huo kwa mujibu wa Profesa Tibaijuka,
 mpaka kati ya Tanganyika na Kongo na hata Malawi, ulikuwa Mashariki ya 
Ziwa na hivyo hata Ziwa Tanganyika, lilipaswa kuwa Kongo.
Alifafanua kuwa katika upimaji, baada ya 
kufanya uamuzi huo wa watawala, hatua ya pili ilikuwa kuunda tume kwenda
 kuhakiki mpaka huo kwa kuzungumza na wenyeji, na kuurekebisha kwa 
kufuata taarifa za wenyeji.
Mwaka 1898 tume hizo zikaundwa, na matokeo yake mipaka Ziwa Tanganyika, Mto Songwe na hata Ziwa Victoria ikawekwa katikati.
Kwa bahati mbaya, mwaka 1914 Vita ya Kwanza
 ya Dunia iliibuka na kusababisha tume hizo kusimama kazi kabla ya 
kupita na kuthibitisha mpaka katika Ziwa Nyasa.
Profesa Tibaijuka aliendelea kuanika 
ushahidi huo, kwamba baada ya vita ya dunia, Ujerumani ilishindwa na 
kupoteza makoloni yake ambayo yalichukuliwa na League of Nations ikiwamo
 Tanganyika ambayo ilitolewa kwa Uingereza kama mwangalizi.
Tanzania imethibitisha katika ushahidi wake
 kuwa, kitendo cha Uingereza kupewa Tanganyika kuwa mwangalizi huku 
Malawi ikiwa koloni lake, kilisababisha tume hiyo kutoendelea na kazi, 
kwa kuwa hakukuwa na umuhimu wa mpaka, wakati mtawala wa Malawi na 
Tanganyika akiwa mmoja.
Kwa mujibu wa Profesa Tibaijuka, Uingereza 
ilikuwa ikipeleka taarifa za uangalizi mara kwa mara League of Nations 
na kabla ya uhuru miaka ya 1950, Gavana wa Tanganyika alipeleka taarifa 
kutaka tume ifanye kazi yake kuhusu mpaka.
Profesa Tibaijuka alisema taarifa hizo ziko
 Geneva, Umoja wa Mataifa, na ujumbe wa Tanzania ulilazimika kwenda 
kupekua katika maktaba ya Umoja huo kupata vielelezo vya taarifa za 
Uingereza kuhusu mpaka, ambazo zimetumika katika ushahidi.
Ushahidi mwingine ambao Profesa Tibaijuka 
alisema utaisaidia Tanzania ni makubaliano ya kimataifa yaliyo chini ya 
Umoja wa Mataifa kuhusu kugawana eneo la maji.
Alisema kwa kufuata makubaliano hayo, haiwezekani watu wa Mbamba Bay, waombe kunywa maji ya Ziwa Nyasa kutoka Malawi
 
No comments:
Post a Comment