Saturday 29 November 2014

Haya hapa majina yaliyoteuliwa na PAC kuandika maazimio ya kuwawajibisha watuhumiwa wa Escrow…


PACBaada ya Spika wa Bunge kuahirisha Bunge mara mbili siku ya leo Novemba 29 ili kuipa nafasi kamati ya PAC iweze kufanya marekebisho ya maneno yaliyoandikwa kwenye maazimio yaliyowasilishwa na Kamati ya PAC, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Zitto Kabwe ametaja majina ya walioteuliwa na Kamati hiyo kuandika maazimio ya kuwajibisha watuhumiwa wa Tegeta Escrow.
 
Zitto Leo

Friday 28 November 2014

Magazeti ya Tanzania leo Nov 28

.
.
;
;
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
DSC06195
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

migogoro ndani ya Bunge la Afrika Mashariki na kilichoamuliwa

Margaret-Zziwa 
Spika wa Bunge la Afrika Mashariki EALA, Margaret Zziwa amesimamishwa kazi na Wabunge wa Bunge hilo kwa kile kinachoelezwa kuwa amekuwa akiendeleza ubaguzi kwenye ajira, ufisadi na pia hana uongozi bora.
Katika mahojiano aliyoyafanya na kituo cha BBC amekana madai hayo na kusema malumbano yanayoendelea ndani ya Bunge hilo yanatokana na siasa za chuki baina ya Wabunge na kusababisha Bunge hilo kutimiza majukumu yake.
Uchunguzi unafanyika ili kujua kama madai yaliyopelekea kumsimamisha yalikuwa na ukweli wowote.

mkusanyiko wa Stori kubwa muhimu za Magazeti ya leo Novemba 28,2014

JAMBOLEO
Wakati mjadala wa Escrow ukiendelea Bungeni Dodoma,zNi halali yako kupata kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia twitter instagram na facebook ukijiunga na mimi kwa imedaiwa kutawala miongoni mwa wabunge ili kuhakikisha wanaotuhumiwa na wizi wa fedha hizo hawawajibishwi kama kamati ya bunge ya hesabu za Serikali PAC ilvyopendekeza.
Wakizungumza kwa nyakati togfauti katika viwanja vya bunge ,baadhi ya wabunge wakiwa wa CCM na wanaounda PAC walionekana dhahiri kutoridhishwa na mwenendo wa mambo yanavyoendesha mara baada ya ripoti hiyo kusomwa.
Mbunge wa Mwibara Kangi Lugola alisema  imebainika safari hii rupia imepenyezwa kila konahali inayosababisha kuteka wabunge wengi na kudhoofisha mjadala.
“Lumbesa ikishaingia mahali hakuna kupitisha uzio,ukishapokea rushwa unakua kipofu,husikii lakini hatukubali jambo hilo.
Hamis Kigwangallah naye alisema ameshangazwa na kamati ya uomgozi ilivyofnya muda wa kuijadili ripoti hiyo kwa kuwa jana jioni manasheria mkuu alitarajiwa kutoa utetezi wake pia Waziri mkuu.
MWANANCHI
Askofu msaidizi wa jimbo la Bukoba Methodius Kilaini amekiri kupokea milioni80.5 kutoka kwa mkurugenzi wa VIP Engeneering,James Rugemarila akisema si mara yake ya kwanza kupokea fedha kuroka kwa mfanyabiashara huyo kwa kuwamara nyingi huwa anachangia  kwa uwazi miradi ya jamii.
Kilaini alisema Rugemarila hupendelea kuchangia miradi ya maendelezo kwa uwazi na si yeye pekee aliyempatia mchango kuna watu wengine wengiambao wamempatia michango na kazi yake yeye ni kuipokea na kuifikisha sehemu husika.
Alisema fedha hizo alizozipokea ni kwa ajili ya miradi inayoendeshwa na kanisa Karoliki na fedha zote anazopokea si siri na kuwatgaka wanaomuhofia kuwa ni miongoni mwa mafisadi wawafate wahusika.
“Ndiyonimepokea fedha na si mara ya kwanza amekua aitoa misaada kila wakati na hii si sirim,wafuateni wezi halisi si mimi”alisema.
MWANANCHI
Bunge la Afrika Mashariki limemsimamisha kwa siku 21 Spika wake Margaret Zziwa huku likifufua hoja ya kumwondoa kiongozi huyo madarakani ambayo iliwekwa kando April1 mw aka huu.
Bunge hilo pia liliafiki kauliya Mbunge kutoka Tanzania AbdulMwinyi ya kumzuia Dk ya kumzuia Spika Zziwa kujihusisha na shughuli zozote za  za nafasi ya Spika mpaka hapo uchunguzi dhidi ya tuhuma utakapokua umekamilikana na kuwasilishwa bungeni.
Uamuzi wa Bunge hilo ulifikiwa juzi mchana ikiwa ni hitimisho la mkutano wa saa nne ambao ulimchagua Mbunge kutoka Uganda Chris Opako kusimamia mchakato huo wa kumwondoa Zziwa madarakani  kwa mujibu wa uendeshaji wa Bunge hilo.
Msemaji wa bunge hilo Bobi Odiko alisema kusimamishwa kwa Spika Zziwa kunamaanishakwamba bunge hilo halitaweza kukutana tena kwa siku chache zilizobakia hadi pale kamati itgakapokua imemaliza kazi yake.
MWANANCHI
Watu 11 wamekufa papo hapo na wengine 25 kujeruhiwa baada ya basi dogo aina ya Coaster kugongana uso kwa uso na lori la mizigo aina ya scania katika kijiji cha Mkanyageni Wilaya ya Muheza,Mkoani Tanga.
Ajali hiyo ilitokea jana saa11 asubuhi wakati basi hilo lili[okua linatoka Tanga kwenda Lushoto na Lori hilo likitokea Lushoto kwendaTanga.
Kaimu Mganga mkuu wa Wilaya Peter Mwankai alisema miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika hospitali teule ya Muheza na tayari maiti saba zimetambuliwa na ndugu zao.
Alisema majeruhi 22 wanaendelea vizuri na wana endelea kupatiwa matatibabu katika hospitalihiyo chini ya uangalizi maalum.
NIPASHE
Jitihada za Serikali kuibadilisha nchi kuwa  miongoni mwa zile zenye malengo makuu ya maendeleo zinawea kutoleta mafanikio kutokana na bajeti ndogo inayotengwa kwa ajili ya kusimamia miradi mbalimbali.
Uwezo huo mdogo wa bajeti umesababisha miradi mingi ya Serikali kusuasua na mingine kufa,ingawa mfumo wa kiutendaji inaonyesha Tanzania imefanya vizuri kwa asilimia90.
Mratibu wa mradi wa Taifa wa kusimamia maendeleo ya Umoja wa soko la pamoja COMESA Cliford Tandaralisema kupitia ripoti ya utendaji imeonyesha kufanya vizuri kwani kwani sekta za umma kama Baraza la Mawaziri,Bunge na Mahakama ni mihili mikuu katika nchi kusimamiwa vizuri hasa kiutendaji.
Inadaiwa kuwa uchumi wa Tan zania ni moja ya uchumiunaokua kwa kasi duniani na kwamba katika miaka10 hadi15 iliyopita uchumi umekua kwa wastani wa asilimia 7.
NIPASHE
Uandikishaji wa wapiga kura katika Jiji la Dar essalaam umekumbwa na vurugu katika baadhi ya maeneo.
Wakazi wa maeneo mbalimbali walisema  ofisi zilizuka katika ofisi za Serikali za mitaa baada ya mawakala wa vyama kuingilia kati na kudai kuwa uandikishaji huo haukufuata utaratibu wa mipaka yao na ziliztulizwa na polisi waliokua wakilinda usalama katika vituo ya uandikishaji ambao walisimamia hadi muafaka upatikane.
Alisema kuwa vurugu hizo zimechukua saa tatu hali iliyochangia kusimamishwa kwa zoezi hilo ili kukaa na mawakala wa vyama na kujadili muafaka wa sehemu yenye matatizo  ya mipaka watajiandikisha wakati mwingine.

Thursday 13 November 2014

Kilichomtokea Mwanamke aliyeongoza mashambulizi ya Westgate Kenya

White Widdow
                                                    Samantha Lewthwaite


Screen Shot 2014-11-13 at 4.07.23 PM
Septemba 21, 2013 ni moja ya siku ambazo zina kumbukumbu nzito ya majonzi kwa watu wa Kenya, kutokana na kupata shambulizi la kigaidi liliposababisha vifo vya watu zaidi ya 60 huku hofu kubwa ikitanda na kupelekea baadhi ya maeneo ambayo huwa na mkusanyiko wa watu wengi Afrika Mashariki ikiwemo Mlimani City Dar kuwekwa ulinzi wa hali ya juu.
Taarifa inayomhusu mtuhumiwa namba 1 wa kesi ya mashambulizi ya jengo la Westgate Samantha Lewthwaite ni kwamba ameuawa kwa kupigwa risasi.
AP_kenya_mall_attack_jt_130921_16x9_992
Hii ni wakati wa shambulio la Westgate.
Taarifa zinasema mtuhumiwa huyu ambaye alikuwa akifahamika kama “White Widow” ameuawa Ukraine katika mapambano ambapo alikuwa akipambana upande wa kikosi cha wapiganaji wa Aidar.
Samantha amekuwa akituhumiwa kuhusika na matukio kadhaa ya mashambulizi ikiwemo la Westgate Kenya mwaka 2013 japo matukio hayo mengi haikuwahi kuthibitika juu ya ushiriki wake.

Ajali ya kwanza kutokea katika majengo marefu ya ghorofa pacha.

Stranded window washers hang on the side of 1 World Trade Center in New York 
Hii inakuwa ajali ya kwanza kutokea wiki moja tangu kuzinduliwa kwa majengo ya ghorofa pacha ya One World Trade Centre, New York Marekani.


Watu wawili wanaofanya shughuli za kusafisha vioo vya majengo makubwa na ghorofa, wamepata ajali wakati wakifanya shughuli hiyo katika moja ya ghorofa za One World Trade Centre na muda mfupi baadaye wakaokolewa na Askari wa Kikosi cha Zimamoto.
b2qxsg5cyaaj9vn-1-480x360

Kamba za lifti ambayo wanaitumia kufanyia kazi hiyo zilinasa na kugoma kufanya kazi wakiwa ghorofa ya 69, wakajikuta wanakaa bila msaada wowote kwa saa moja na nusu, huku wapita njia walioshtushwa na tukio hilo wakiendelea kuwapiga picha ambazo zimeenea mitandaoni.
A stranded window washer is pulled into 1 World Trade Center in New York
US-ACCIDENT-OFFBEAT

MAMBO YA SIMU ZA MKONONI NA MATUMIZI YA MUDA WA MAONGEZI

DSC05550 
Watumiaji wengi wa huduma ya simu za mkononi wamekuwa wakilalamikia wizi wa pesa unaofanywa na baadhi ya makampuni hayo, leo katika kikao cha Bunge Dodoma Serikali  imesema inatambua kuhusu wizi unaofanya na baadhi ya makampuni ya simu za mkononi na kutoa tamko namna ambavyo imejipanga kukabiliana na wizi wa aina hiyo.
Akitoa tamko hilo Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia January Makamba amesema Serikali itaanzisha kituo maalum cha kushughulikia malalamiko hayo CCC, kitakachokuwa kinasimamiwa na TCRA.
Akiuliza swali kuhusiana na jinsi Serikali ilivyojipanga  kukabiliana na wizi huo Mbunge wa Konde Khatib Said Haji amesema; “… Wizi huu unaofanywa na makampuni ya simu si wizi mkubwa kama ule wa ESCROW..  ni wizi mdogo mdogo unaowaibia Watanzania elfu tano elfu tatu lakini kwa ujumla wake, Mpemba aliyeko Konde akiibiwa elfu tatu, Mnyamwezi wa Tabora elfu mbili, Ukizijumlisha ni mamilioni ya shilingi wanaibiwa Watanzania… Leo watu hao elfu tatu elfu mbili unawaambia wapeleke malalamiko yao, gharama hiyo umeikadiriaje hata mtu huyo akadai malalamiko ya elfu tatu..
.. Hivi serikali yenu makini imekuwa wapi muda wote mpaka kukiri kama Watanzania wamekuwa wakiibiwa na bila wenyewe kujijua?, na bado hamna hatua mlizozichukua, ni nani aliyeko nyuma ya pazia hili la kuibia Watanzania na ninyi mkaridhia ama ni yale yaliyosemwa kama CCM ina fund katika wizi huu..?”- Khatib Said Haji.
Akijibu swali hilo Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia January Makamba amesema; “…Napenda nikiri tatizo la wizi au dhuluma kwa wateja lipo na ndio lililopelekea tukaweka hizi kanuni ambazo zinaweka adhabu na hatua za kuchukua katika kuchukua katika kudhibiti wizi huo.. Licha ya utaratibu wa kawaida wa kulalamika katika makampuni  ya simu, kwa sababu moja ya matakwa ya sheria ni kwamba kampuni za simu zinapaswa kuweka utaratibu wa kuhudumia watekja wake, lakini tumebaini kwamba utaratibu huo una matatizo, unaweza ukapiga  simu muda mrefu isipokelewe, unaweza kuambiwa usubiri na wakati unasubiri kulalamika pia unakatwa..
Kwa hiyo Serikali inafahamu hilo, pamoja na hatua tulizozichukua ni kuweka ule mtambo wa kufuatilia mawasiliano ambao moja ya kazi yake sio kufuatilia tu mapato lakini ubora wa mawasiliano.. Kwa kutambua kuwa makampuni ya simu haya wakati mwingine yanachelewa wakati mwigine yanapuuza wateja, kituo hiki ambacho tunakianzisha namba zake zitasambazwa kila mtu atakuwa nayo, kwa hiyo huna haja kusafiri kufuatilia shilingi elfu mbili elfu tatu elfu tano. Kutakuwa na namba ambayo ni bure kupiga..”- January Makamba.
Kila utakapopiga kulalamika utapewa namba maalum ya lalamiko lako, na lisiposhughulikiwa hata kitengo cha kampuni ya simu kutoshughulikia lalamiko lako na yenyewe itakuwa sababu ya makampuni hayo kuadhibiwa..”- January Makamba.

AJALI TENA

MWANGA
Habari zilizotufikia kutoka Mwanga Mkoani Kilimanjaro zinasema kuna ajali mbaya imetokea maeneo ya Mwanga wakati basi la kampuni ya Mbazi Travellers lililokua likitokea Arusha kuelekea Dar es salaam kupinduka.

Taarifa  zinasema ajali hiyo ilitokea baada ya basi hilo kujaribu kulipita basi jingine huku kukiwa hakuna mtu aliyepoteza maisha lakini inasemekana kuna idadi kubwa ya majeruhi ambao walikimbizwa katika hospitali ya KCMC Moshi

Wednesday 12 November 2014

BASI LA WIBONELA LAPATA AJALI KAHAMA

Screen Shot 2014-11-12 at 11.54.22 AM
Screen Shot 2014-11-12 at 11.54.36 AM
Screen Shot 2014-11-12 at 11.54.44 AM
Screen Shot 2014-11-12 at 11.54.52 AM
Screen Shot 2014-11-12 at 11.18.07 AM
Screen Shot 2014-11-12 at 11.17.42 AM
Ni Basi la Wibonela Express linalofanya safari zake kati ya Kahama – Dar ambalo lilipinduka baada ya kutoka stand kuu ya kahama kilometa chache toka stand hiyo kwenye eneo la Phantom ambapo taarifa kutoka Polisi zinasema waliofariki ni watu wanne.
Taarifa za awali zinasema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi.
Screen Shot 2014-11-12 at 11.17.48 AM

Screen Shot 2014-11-12 at 11.17.55 AM

Screen Shot 2014-11-12 at 11.18.01 AM

Screen Shot 2014-11-12 at 11.17.35 AM

Screen Shot 2014-11-12 at 11.17.29 AM

Screen Shot 2014-11-12 at 11.17.21 AM

Screen Shot 2014-11-12 at 11.17.10 AM

Screen Shot 2014-11-12 at 11.18.13 AM