Viongozi 
waliovuliwa nyadhfa zao ni Mwenyekiti wa jimbo la Kahama Israel 
Barikiel, Katibu wa Jimbo Vicent Kilukilwa, Katibu Mwenezi wa jimbo 
Bobson Wambura, Mwenyekiti Bawacha Kasigwa Adram na Mwenyekiti Bavicha 
Benedict Shija.
Katika Barua 
yake aliyoiandika kwa viongozi hao, Nzemo amesema viongozi hao 
wanakabiliwa na tuhuma za kikiuka tamko la kamati kuu ya chama 
lililowazuaia wanachama wote kushirikiana na aliyekuwa naibu katika mkuu
 wa chama hicho Zitto Kabwe.
Tuhuma 
zingine ni kushiriki kampeni za uchaguzi mdogo katika kata ya Ubagwe 
kupitia chama cha TADEA, huku viongozi hao wakipita na kujinadi kuwa 
wako tayari kumfuata Zitto popote atakapokuwa.
Aidha Nzemo 
amesema viongozi hao wamekuwa wakitumia nembo ya CHADEMA kunadi chama 
kingine cha Alliance for change and Transparency (ACT), kinyume cha 
maadili ya CHADEMA katika katiba yake ya mwaka 2006.
Nzemo amesema
 kutokana na tuhuma hizo na zile zilizotolewa na baraza la mashauriano 
wilaya ya Kahama, viongozi hao wanatakiwa kukabidha ofisi na vifaa vya 
chama kwa baraza la wazee jimbo la Kahama mara wapatapo barua hizo.

 
No comments:
Post a Comment