Tuesday 25 February 2014

MAREKANI YACHUKIZWA NA RAISI MUSEVENI KUSAINI MUSWADA WA SHERIA KALI JUU YA WAPENZI WA JINSIA MOJA


John Kerry asema Uganda inakiuka haki za binaadamu
Marekani haikufurahishwa na hatua ya Uganda kuidhinisha sheria dhidi ya wapenzi wa jinsia moja.

Waziri wa mashauri ya Kigeni wa Marekani, John Kerry amesema tangu Uganda iidhinishe mswada huo miaka minne iliyopita, Marekani ilieleza wazi kwamba sheria hiyo inakiuka jukumu la kuhakikisha kuwepo haki za binaadamu ambalo tume ya haki za binaadamu Uganda inatambua linaambatana na sheria ya Uganda.

Kerry amesema,' Baada ya kuidhinishwa sheria hii, tunaanza ukaguzi wa ndani wa uhusiano wetu na serikali ya Uganda, kuhakikisha kwamba pande zote za uhusiano wetu, ukiwemo miradi ya msaada, zinapinga sera na sheria zinazowaonea watu na tuwe na uhusiano unaodhihirisha maadili yetu'.
Tamko hilo limetolewa siku moja baada ya rais Yoweri Museveni kukaidi shinikizo la kimataifa na kutia saini sheria hiyo iliyo zusha mzozo, inayoharamisha mapenzi ya jinsia moja Uganda, hatua iliyozusha hisia kali.
Baadhi ya mataifa ya magharibi tayari yanatishia kukatiza msaada wa moja kwa moja kwa serikali ya Uganda.
Marekani inasema kuidhinishwa kwa sheria hiyo kunatishia hatari ya kurudi nyuma katika uwajibikaji wa Uganda kulinda haki za raia wake na kutishia jamii ya wapenzi wa jinsia moja Uganda.Chanzo BBC Swahili

Kikwazo kingine kutoka kwa Chris Brown.

chris-brown-2013-650-430-b
February 22 Chris Brown ametangaza siku atakayoachia rasmi album yake ambayo kwa mwaka jana ni mara kadhaa imekua ikihairishwa kutokana na sababu mbalimbali,jina la ulbum hiyo ni X ambayo ina tafsiri nyingi huku wengine wakidai ni kama maalum kwa X wake.
Leo february 25 Chrss Brown ametweet maneno haya>>My old manager is leaking my NEW album music and refuses to give me my back up hard drive to sabotage my album.That’s F’d up G!’.
chris-tweet

Tweet hiyo baadae aliifuta Chris Brown kwa sasa kamaliza ile program yake ya kukaa rehab ya siku 90 ambayo iliamuriwa na mahakamam mwaka 2013,bado maswali yapo juu ya album hiyo kama itatoka may 05 kama alivyotangaza jana au itashindikana kwa kile alichokiandika kuhusu kuvujishwa kwa nyimbo hizo na huyo aliyekua meneja wake ikiwa ni pamoja na kugoma kumpatia back up hard drive yake.
Chris Brown  February 22 alitweet na kutoa rasmi tarehe ya kuachiwa album hiyo yake hiyo aliyoipa jina la  X ambayo ilikua itoke July 2013.

Monday 24 February 2014

AKAMATWA AKIDAIWA KUUZA NYAMA YA BINADAMU

Mkazi wa Kijiji cha Kihinga, Kata ya Bugarama wilayani Ngara mkoani Kagera(jina tunalo), anashikiliwa katika kituo kidogo cha polisi cha kata hiyo baada ya kutuhumiwa kuuza kilo moja ya nyama ya binadamu kwa Sh100,000.
Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kihinga, Hassan Mohamed alisema kuwa jana saa mbili usiku, wananchi walipeleka fedha nyumbani kwake kununua nyama hiyo na alipowaona alikimbia na wananchi hao kwa hasira walimkimbiza ili kumuua na hapo hapo kuunguza nyumba yake.
“Mgambo ndio walimnusuru asiuawe na wananchi wenye hasira kali na alikimbizwa kituo kidogo cha polisi Kata ya Bugarama ili kuokoa maisha yake “.
Akizungumza na gazeti hili, Kamanda wa mgambo wa kijiji hicho, Emanuel Kaloli alisema wananchi waliandamana baada ya kusikia taarifa za kuwapo mtu anayeuza nyama ya binadamu na kutaka kuhakikisha ukweli huo.
Alisema baada ya wananchi kufika, walianza kumshambulia na kutaka kumuua, lakini wanamgambo wa kitongoji walifika kisha kumuokoa mtuhumiwa na hatimaye kumfikisha kituo cha polisi kwa ajili ya usalama wake.
“Kijana aliyefahamika kwa jina la Man Balyamwabo mkazi wa Shina la Kalenge katika kitongoji hicho, ndiye aliyeambiwa kuwa angeuziwa nyama hiyo ya binadamu na kuleta taarifa katika uongozi wa kijiji ili uweze kuchukua hatua zaidia”.Alisema Kaloli.
Alisema nyumba aliyounguziwa pamoja na mali iliyokuwamo ndani hasa maharage, mavazi na vitu vinginevyo inakadiriwa kuwa na thamani ya Sh2.6milioni. Pamoja na kuwepo kwa tukio hilo, baadhi ya wananchi walisema mtuhumiwa inasemekana ni raia wa nchi jirani ya Burundi na alianza kuishi katika kitongoji hicho tangu mwaka 1981 kama kibarua wa kilimo kwenye mashamba.
Taarifa zinasema kuwa katika kuishi kwake na ndugu yake aliyefahamika kwa jina la Kahungu walikuwa wakituhumiana kwa uchawi na ilifikia mahala wakatofautiana na kaka yake ambaye alirejea kwao.
Polisi wilayani Ngara imethibitisha kumpokea mtuhumiwa huyo na kwamba linafanya mahojiano ya kina kwa kushirikiana na viongozi wa kijiji ili kubaini ukweli wa tukio hilo

MAGAZETI YA LEO JUMANNE TAREHE 25.02.2014


DSC 0001 573e9

DSC 0008 4be0eDSC 0003 5a81c
DSC 0002 1669fDSC 0004 50a13
DSC 0005 bf086
DSC 0006 e425d
DSC 0007 7c36d
DSC 0009 86ee1
DSC 0010 6b76d
DSC 0011 8e143

MILIPUKO YA MABOMU YARINDIMA Z’BAR

bomu_b1855.png

Zanzibar. Watu wanne wamejeruhiwa baada ya milipuko minne inayoaminika kuwa ni mabomu kutokea katika maeneo matatu tofauti Zanzibar.
Katika moja ya matukio hayo, watu wanne walijeruhiwa, mmoja akikatika mguu, katika eneo la Unguja Ukuu, Mkoa wa Kaskazini Unguja. Majeruhi wawili wamelazwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja, Unguja.
Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Mkoa wa Kusini Unguja, Hamad Said Masoud alisema mlipuko wa kwanza ulitokea juzi katika eneo la Fuaoni Maili Nne wakati watu wasiojulikana waliporusha kitu kinachoaminika kuwa ni bomu wakati waumini wa Kanisa la Evangelist wakiendelea na ibada ya Jumapili.
Kamishna wa Polisi Zanzibar, Hamdan Omar Makame alisema tukio la juzi, kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu kilirushwa wakati waumini wa kanisa hilo wakiendelea na ibada na kutoa mlipuko na kishindo kikubwa. Alisema wakati wakiendelea na uchunguzi wa tukio hilo, milipuko mingine mitatu ilitokea jana.
Katika mlipuko wa kwanza kwa jana uliotokea saa 6.30 mchana katika kituo kimoja cha fundi vyuma aliyetambulika kwa jina la Juma Abdallah huko Unguja Ukuu ndiko kulikokuwa na watu waliojeruhiwa.
Waliojeruhiwa katika tukio hilo ni Pandu Haji Pandu aliyekatika mguu na Shaaban Khamis Ibrahim ambaye aliumia sehemu za kiuno.
Hamad alisema mtu mmoja aliokota chuma kizito na kukipeleka kwa fundi akitaka atengenezewe nanga kwa ajili ya uvuvi.

ANAYEONA POSHO HAIMTOSHI AFUNGASHE VIRAGO’


bunge_4f64b.jpg
Dodoma. Wizara ya Fedha imepigilia msumari maombi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba ya kutaka waongezewe posho na kusema anayeona ameacha kazi inayomlipa zaidi kwenda bungeni afungashe virago na kuondoka.
Msimamo huo umekuja siku moja tu baada ya gazeti hili kudokeza kuwa madai ya wajumbe wa bunge hilo kutaka waongezewe posho kutoka Sh300,000 za sasa kwa siku, yamegonga mwamba baada ya kamati iliyoteuliwa kuchunguza uhalali wake kusema kiwango hicho kinatosha.
Mwenyekiti wa muda wa bunge hilo, Pandu Kificho alisema jana bila kutaja viwango, kuwa ripoti ya kamati hiyo imewasilishwa kwa Rais Jakaya Kikwete kwa uamuzi.
Madai ya wajumbe kutaka waongezewe posho, yamechafua hali ya hewa ndani na nje ya Bunge, huku baadhi ya wananchi wakipaza sauti zao na kumsihi Rais Kikwete alivunje bunge hilo iwapo wajumbe watashikilia msimamo wa kutaka nyongeza ya posho

WATU SABA WAFARIKI DUNIA MKOANI IRINGA

 

Watu saba wamefariki dunia katika matukio sita tofauti mkoani Iringa likiwemo la watoto wawili kufariki wakiwa wanaogelea kwenye dimbwi la maji lililopo kijiji cha Mkungugu tarafa ya Isimani.
Akizungumza  ofisini kwake kaimu kamanda wa polisi Mkoani Iringa Mratibu mwandamizi Peter Kakamba alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea mnamo tarehe 23 februari majira ya saa 12:30 jioni.
Kaimu Kakamba aliwataja watoto hao ni Nestory Luhala(8) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la pili pamoja na Junior Luhala(5).
Tukio lingine mwanafunzi wa miaka 14 ajulikanaye kwa jina la Iginasi Ngalembule mkazi wa Isuka  kata ya Mtitu wilayani Kilolo afariki dunia baada ya kupigwa na radi.
Kaimu Kakamba alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea mnamo tarehe 22 februari majira ya saa 11 kamili jioni.

MVUA ZASABABISHA MADHARA MAKUBWA BARABARA RUPINGU - LUDEWA ,MBUNGE AKWAMA KUFANYA ZIARA ASHINDA AKIFUNGUA BARABARA

Wananchi na  msafara  wa  mbunge  wa  jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe wakifungua barabara ya  Rupingu -Ludewa  iliyofunikwa na kifusi baada ya mvua kubwa  kunyesha kwa zaidi ya wiki moja mfululizo sasa barabara  hiyo  ipo katika matengenezo makubwa na TANROADS mkoa wa Njombe kwa kutegewa kiasi cha Tsh milioni 400.CHANZO FRANSIS GODWIN 
Gari la Mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe  likipita kwa shida katika barabara ya Rupingu -Ludewa jana
Mbunge wa  Ludewa Deo Filikunjombe akitazama sehemu ya barabara ya Rupingu - Ludewa  inayoporomoka kutokana na mvua  kubwa  zinazoendelea  kunyesha
Mbunge wa Ludewa  Deo Filikunjombe akionyesha madhara ya  Mvua yaliyopelekea barabara ya Rupingu -Ludewa  kuharibika

RANGI NYINGINE YA WANYAMA WA FEO HII HAPA KITU KIPYA THANX GOD KIMEFIKA SALAMA TOKA CHINA




MAPENZI YA JINSIA MOJA UGANDA SASA NI MARUKUFUKU!!!!!!!!

Moses mwanamume anayeshiriki mapenzi ya jinsia moja atafuta hifadhi nchini Marekani
Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametia saini mswada wenye utata unaotoa adhabu kali kwa watakaopatikana wakishiriki mapenzi ya jinsia moja.
Rais Museveni alitia saini mswada huo nyumbani kwake katika hafla iliyoshuhudiwa na maafisa wakuu wa serikali pamoja na wandishi wa habari.
Mswada huo ambao sasa utakuwa sheria, unatoa adhabu ya kifungo cha miaka 14 jela kwa wale watakaopatikana na hatia kwa mara ya kwanza,
Adhabu ya maisha jela itatolea kwa watu watakaopatikana na hatia ya kushiriki mapenzi ya jinsia moja zaidi ya mara moja kati ya watu wawili waliokubaliana kufanya hivyo.
Adhabu hiyo pia itatolewa kwa wale wanaopatikana na hatia ya kuwahusisha watoto katika vitendo hivyo, walemavu au kumuambikiza mtu virusi vya Ukimwi.
Mswada huo umepigiwa debe sana nchini Uganda, lakini mashirika ya kimataifa ya kutetea haki za binadamu yameulaani.

MWANAMKE AKAMATWA AKITUPA MTOTO MCHANGA CHOONI HUKO MBEYA



Rukia Fungameza(20) mkazi wa mtaa wa Ilembo Kata ya Iwambi Anaetuhumiwa kutupa mtoto chooni
 
 Hii ndilo shimo la choo alimotumbukizwa mtoto huyo.

 Wakina mama wakilia kwa uchungu
 
Mwenyekiti wa mtaa huo Juma Mbuza mwenye Flana ya bluu akiwa na barozi kushoto na mashuhuda wengine wakimsikiliza mwenyekiti huyo.
Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Rukia Fungameza[20]mkazi wa mtaa wa Ilembo Kata ya Iwambi anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya kwa tuhuma za kutupa chooni kichanga jinsi ya kiume na kusababisha kifo chake.

Mwenyekiti wa mtaa huo Juma Mbuza amesema walimtilia shaka mtuhumiwa Februari 18 mwaka huu katika klabu ya pombe za kienyeji baada ya kutoonekana na ujauzito,ndipo walipomuuliza kulikoni naye kudai kuwa amejifungua lakini mtoto yupo nyumbani.

Kauli hiyo haikumridhisha Mwenyekiti huyo ndipo alipoamua kumtafuta balozi wake aitwae Daud Dule na kumuuliza mtoto yupo wapi ndipo alipoanza kuwa na wasiwasi hali iliyowalazimu kumkamata kutoa taarifa kituo cha Polisi Iyunga ambapo kabla ya kufika Kituoni majira ya saa kumi na moja jioni mtuhumiwa alikiri kujifungua na kutupa kichanga chooni Februari 18 mwaka huu

PICHA ZA USTADHI ATENGANISHA KICHWA NA MWILI WA MTOTO JAMALI SALUM LIPAKALE HUKO MBAGALA CHARAMBE HIZI HAPA !!

mwili wa marehemu mtoto Jamali aliechinjwa na ustadhi mbagala charambe mianzini














mwili wa marehem ustadhi mohamed kurangwa aliemchinja mtoto ukishushwa katika hospitali ya Temeke

baadhi ya familia wakiwa katika msiba



baadhi ya wakazi wakichungulia nyumba lililotokea tukio la mauaji ya kikatili