Wednesday 29 January 2014

UHARIBIFU WA MAZINGIRA MANISPAA YA SONGEA.


Tatizo la uvunjaji wa kokoto na uharibifu wa mazingira katika mto Ruhila Manispaa ya Songea linahatarisha ukosefu wa maji kwa matumizi ya kilimo na nyumbani .
Baadhi ya kokoto ambazo tayari zimepasuliwa kwenye miamba iliyopo mto Ruhila,na kusababisha uharibifu wa mazingira

MABASI YA MWAKYEMBE YAANZA KUTESA MUJINI BONGO LIVE!!


Mmoja ya basi la mwendo kasi likikatiza mtaa wa Lumumba ikiwa sehemu ya majaribio ya mabasi hayo ambayo yanaaminika yataondoa kabisa tatizo la usafiri katika jiji la Dar.

Matokeo ya mechi zilizochezwa January 28 yapo hapa.

matokeo

Kurasa za mwanzo na mwisho magazetini leo January 29 2014 kwa hisani ya brog rafiki

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

Monday 27 January 2014

SERIKALI YAPUNGUZA GHARAMA ZA KUUNGANISHA UMEME


                                                 Prof. Sospeter Muhongo
*Ni kwa wanavijiji wanaoishi jirani na bomba la gesi Mtwara - Dar
 
SERIKALI imeamua kupunguza kwa kiasi kikubwa bei ya kuunganisha umeme majumbani na kufikia sh. 27,000/ kwa wanavijiji wanaoishi kwenye maeneo ambayo bomba la gesi linapita.
 
Hatua hiyo imetangazwa jana (Jumapili, Januari 26, 2014), na Waziri wa Nishati na Madini,Prof. Sospeter Muhongo wakati akizungumza na wanakijiji wa Mangaka wilayani Nanyumbu, mkoani Mtwara kabla ya kumkaribisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda azindue mradi wa umeme kwenye wilaya hiyo.
 
“Jana Waziri Mkuu aliagiza tutafute namna ya kuwasaidia wananchi wanaoishi jirani na njia ya bomba la gesi. Nami nilikaa na wasaidizi wangu jana usiku na kufanya hesabu na tukaamua tuweke kiwango hicho kwa ajili ya wakazi hao,” alisema.
 
Alisema katika mikoa mikoa mingine gharama za kuunganisha umeme ni sh. 177,000/- lakini kwa mikoa ya Lindi na Mtwara gharama hizo zilishushwa na kufikia sh.99,000/-. “Lakini sasa hawa wenzetu tumewapa upendeleo zaidi na tumewapunguzia gharama hizo hadi sh. 27,000/-,” alisema huku akishangiliwa.
 
Gharama hizo ni maalum kwa ajili ya wakazi waishio jirani na bomba hilo linaloanzia Mtwara hadi Dar es Salaam kupitia mikoa ya Lindi na Pwani.

BAADA YA MBINGA - DSM SASA NI ZAMU YA SONGEA - DOM.KAENI MKAO WA KULA MFALME WA KUSINI ANAKUJA !!!!!!


Habari zilizothibitishwa hivi punde na mkurugenzi mkuu wa Super Feo Express kuanzia muda wowote toka sasa kampuni ya Super Feo itaanza safari mpya ya SONGEA-DODOMA via MTELA tutaendelea kuwajuza zaidi kinachoendelea

Hii ndiyo namba aliyopewa Juan Mata ndani ya Man United

Makabidhiano hayo yamefanyika kati ya Mata na kocha David Moyes.
ata


mata
Juan Mata amekabidhiwa rasmi jezi ya Manchester united yenye namba 8 mgongoni.

Choo cha Birdman kilichotengenezwa na dhahabu, kichokadiliwa kuwa na thamani ya $1mil hiki hapa.


birdam2DSa


Birdman boss wa record label ya YMCMB ambaye mara nyingi huwa anajisifia kwa matumizi yake makubwa ya pesa kwenye vitu luxury, ameendeleza hivyo vitendo  vya kufanya matumizi makubwa ya pesa.
Hivi karibuni ame-share picha ya choo chake ambacho kime-kuwa covered na material ya dhahabu pande zote.
Mfuniko wake na sehemu ya juu ya choo hicho ni dhahabu tupu na sehemu nyingine yote hautaweza kukiona hicho choo kwasababu kimefunikwa na dhahabu.
Gharama yake inakadiliwa na kuwa na thamani ya dola millioni moja.
birdama



birdam2a

Sunday 26 January 2014

BREAKING NEWSSSS MKUU WA POLISI WILAYA (OCD) IRINGA APATA AJALI


Askari  walikuwa  wakielekea katika mkutano   wa uzinduzi wa  kampeni  za CCM kata  ya  Nduli Iringa mjini wakitazama gari  ambalo alikuwa akiendesha  OCD Iringa  lililopata  ajali majira ya saa 10 jioni  jumapili japo hakuna  aliyepoteza maisha  ktk ajali hii iliyotokea  kona  la Mgongo barabara ya Iringa-Dodoma
wasomi  wa  chuo  kikuu cha Iringa wakitazama  ajali hiyo ambayo dereva  wake OCD Iringa  alinusurika  kifo na  kuumia mkono  wake  kiasi

ABANIKWA KAMA KUKU, NI BAADA YA KUTUHUMIWA KUIBA BODABODA MAFINGA


Ezekiel Kaganga
Ezekiel Kaganga (29) mkazi wa Mjimwema Mafinga, wilayani Mufindi mkoani Iringa amelazwa katika hospitali ya wilaya ya Mufindi mjini Mafinga baada ya kubanikwa kwenye moto kama kuku akituhumiwa kuiba pikipiki (bodaboda).
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi amewataja watu wawili wakihusishwa na tukio hilo la kinyama.
Aliwataja waliokamatwa kuwa ni ni Alex Ludago (28) na Steven Michael (29) wote wakazi wa MET mjini Mafinga.
Akisimulia jinsi tukio lilivyokuwa katika wodi namba tano ambako amelazwa Kaganga alisema anafahamiana na watuhumiwa hao na kabla ya tukio hilo Januari 7, mwaka huu walikuwa pamoja wakinywa bia katika moja ya maduka ya kuuzia pombe mjini Mafinga.
Alisema Januari 8 mwaka huu alipokea taarifa katika duka hilo la pombe lililopo katika eneo la mashine ya mpunga kwamba kuna pikipiki ilipotea katika mazingira ya kutatanisha baada ya yeye kuondoka katika eneo hilo siku iliyopita.
Katika majibu yake kwa mmoja wa watuhumiwa hao alisema hajui lolote kuhusu kupotea kwa pikipiki hiyo.
 
Anavyoonekana majereha ya mgongoni
 “Jamaa hao hawakuridhishwa na majibu yangu na Ijumaa ya  Januari 12 alikamatwa na Polisi akihusishwa na tukio hilo na akatoka Januari 17,” alisema.
Alisema baada ya kutoka Polisi alikaa siku tatu uraiani na ndipo alipokamatwa na vijana hao na kupelekwa katika msitu wa Lumwago nje kidogo ya mji wa Mafinga.
Katika msitu huo alifungwa kamba, kupigwa viboko na baadaye alining’inizwa juu ya mti huku moto ukiwa umechomwa chini yake.
Sehemu ya miguu yake
“Nilibanikwa kama kuku, moto ukiwa chini mie nikiwa nimefungwa juu ya miti; niliachwa hapo kwa siku mbili,” alisema.
Alisema baada ya siku mbili alihamishwa kutoka katika msitu huo na kupelekwa eneo la machijio mapya na kumwagiwa mafuta ya taa ili achomwe na moto na kundi la watu wanaokadiriwa kuwa saba.
“Nikiwa mahututi walinichukua na kunipeleka kituo cha Polisi kabla sijaletwa hapa hospitalini nako endelea kupata matibabu,” alisema.
Aliyata maeneo ambayo ameungua sana kuwa ni mgongoni, makalioni, mikononi, ubavuni, miguuni na shingoni.
Kaka wa Kaganga, Aizaki Kaganga alisema “mdogo wangu anaendelea kupata matibabu, na hali yake sio mbaya sana japokuwa hawezi kutembea.”
Alisema alipokea taarifa ya kupotea kwa mdogo wake  kuhusishwa na tukio hilo na akawaahidi watuhumiwa wamsubiri  arudi kutoka safarini Arusha ili alipe pikipiki hiyo.
“Hata hivyo vijana hao hawakuwa na subira hiyo na badala yake wakamfanyia unyama waliofanya,” alisema.
Kamanda Mungi alisema jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo pamoja na kuwasaka watuhumiwa wengine waliohusika na tukio hilo. 
 
Akifarijiwa na kaka yake