Thursday 20 March 2014

Baada ya Zuma kugundulika kutumia vibaya fedha za serikali, hiki ndicho walichosema chama chake

0,,16458368_303,00Chama tawala nchini Afrika ANC kimetoa kauli yake kuhusu tuhuma za utumizi mbaya wa pesa za Umma dhidi ya Rais Jacob Zuma.
Katibu mkuu wa chama hicho, Gwede Mantashe, amesema kuwa afisa yeyote aliyehusishwa na makosa yoyote, lazima akabiliwe na sheria.
Lakini amepuuzia mbali wito wa Rais Zuma kuondolewa mamlakani kwa kura ya wabunge au hata kujizulu.
Hapo jana mdhibiti wa mali ya umma,Thuli Madonsela, alisema kuwa Zuma alitumia sehemu za pesa za umma zilizotengewa ukarabati wa nyumba yake kwa mambo yake binafsi.
Thuli Madonsela, aliamuru Rais Zuma kulipa pesa za ziada alizotumia za umma kukarabati nyumba yake ya kifahari, akisema kuwa alijinufaisha na pesa za umma kwa njia isiyofaa.
Ukarabati huo, ulijumuisha bwawa la kuogelea, kliniki binafsi na eneo la helikopta kuweza kutua.
Chama hicho kimesema kuwa ripoti hiyo imetolewa wakati usiofaa nchi hiyo ikijiandaa kwa uchaguzi mkuu mwezi Mei.
SOURCE: BBC

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI TAR 20.03.2014 VICHWA VIKUBWA KIFICHO AMKANA WARIOBA,JK APIGWA KOMEO NA SILAHA NZITO ZA UGAIDI ZANASWA





DSC 0196 ee1d6
DSC 0197 f826f
DSC 0198 9e073

DSC 0200 e2f0f
DSC 0201 9a332
DSC 0202 17ccb
DSC 0203 c36d6
DSC 0204 bb81c
DSC 0205 01fa0
DSC 0206 9b5a1

Mgogoro Ziwa Nyasa sasa kuamuliwa Leo Maputo

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard Membe.
Maamuzi ya mwisho ya usuluhishi wa mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa kati ya Tanzania na Malawi yanatarajiwa kutolewa kesho na kutwa.
Mchakato wa kesi yake hadi sasa umedumu kwa takribani miaka miwili sasa.
Maamuzi ya mwisho ya usuluhishi huo yanatarajiwa kufanywa na jopo linaloundwa na Marais wastaafu watatu kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini na Mashariki mwa Afrika ambao ni Mwenyekiti waka ni Joachim Chissano (Msumbiji), Thabo Mbeki (Afrika Kusini) na Festus Mogae (Botswana), huku wakishirikiana na wanasheria na wataalam wa masuala ya migogoro ndani ya jumuiya hiyo.
Akizungumza na NIPASHE jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Kitengo na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mindi Kasiga, alisema jopo hilo la usuluhishi wa mpaka kati ya Tanzania na Malawi, katika Ziwa Nyasa, linatarajia kutoa taarifa rasmi ya usuluhishi kwa siku mbili mfululizo kuanzia kesho hadi kesho kutwa katika mji mkuu wa Msumbiji, Maputo.
Mbali na jopo hilo, pia mawaziri wa Mambo ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, kutoka nchi za Tanzania na Malawi, wanatarajia kuhudhuria kikao hicho nyeti cha siku mbili kwa ajili ya kupokea taarifa hiyo ya maamuzi ya mwisho ya usuluhishi.
Jopo la wataalam na wanasheria wa masuala ya mipaka toka ndani ya jumuiya hiyo ambao watashirikiana na Marais hao wastaafu katika kutoa hatima ya usuluhisho huo linaundwa na Jaji Raymond Ranjeva, Jaji mstaafu wa ICJ; Profesa George Kanyeihamba, Jaji mstaafu wa Mahakama Kuu ya Uganda na Jaji Baney Afako, Mshauri wa Masuala ya Sheria kwenye Umoja wa Afrika kuhusu mgogoro wa mpaka wa Sudan. 
Wengine ni Profesa Martin Pratt, Mkurugenzi wa Utafiti wa Jiografia na Mipaka; Dk. Dire David Tladi, Mjumbe wa Kamisheni ya Sheria ya Umoja wa Mataifa; Miguel Chissano, Kiongozi wa Chuo kinachoshughulikia mipaka ya Baharini na Nchi Kavu pamoja na Dk. Gbanga Oduntun, Profesa wa Sheria na Mjumbe wa Kamisheni ya mgogoro wa mpaka kati ya Nigeria na Cameroon.
Kabla ya kufanyika kwa matukio hayo mawili mjini humo mwezi uliopita, Tanzania na Malawi kwa nyakati tofauti, ziliitwa na jopo hilo kuhojiwa juu ya taarifa zao za ushahidi wa umiliki halali wa ziwa hilo zilizowasilisha kwao na mawaziri wa mambo ya nje na wa pande hizo mbili Novemba, mwaka jana.
Julai, mwaa juzi, Rais wa Malawi, Joyce Banda, mara baada ya kuapishwa kushika kiti hicho kufuatia kifo cha mtangulizi wake, Bingu wa Mutharika, aliibua mgogoro huo kwa kutoa leseni kwa kampuni mbili za kigeni, kutafuta mafuta katika eneo la Ziwa ambalo linamilikiwa na Tanzania, kwa madai ya kwamba ziwa hilo lote lipo upande wake.
Mpaka wa Ziwa Nyasa kati ya Tanzania na Malawi, unaotambuliwa na sheria za kimataifa ni ule unaopita kati ya ziwa hilo, ambao ulianza kutumiwa na raia wa nchi hizo mbili miaka mingi iliyopita kwa kila upande kumiliki asilimia 50 ya Ziwa.

MTOTO WA MIAKA 7 AFARIKI KWA KUPIGWA NA BABA YAKE MZAZI

DSC00207“PRESS RELEASE” TAREHE 20.03.2014.  
  • MTOTO WA MIAKA 07 AFARIKI DUNIA BAADA YA KUPIGWA NA BABA YAKE MZAZI.
  • MTU MMOJA AUAWA BAADA YA KUPIGWA NA KUNDI LA WANANCHI KWA TUHUMA ZA WIZI
  • MTEMBEA KWA MIGUU AFARIKI DUNIA BAADA YA KUGONGWA NA GARI KATIKA AJALI YA BARABARANI.
  • JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA RAIA WA KIGENI WATANO KWA KOSA LA KUINGIA NCHINI BILA KIBALI.
KATIKA TUKIO LA KWANZA:
MTOTO AITWAYE IREENE MARCO MBEMBELA (07) MWANAFUNZI CHEKECHEA SHULE YA MSINGI MIGOMBANI NA MKAZI WA SOGEA ALIFARIKI DUNIA WAKATI AKIENDELEA KUPATIWA MATIBABU KATIKA KITUO CHA AFYA TUNDUMA.
MAREHEMU ALIPIGWA KWA KUTUMIA FIMBO SEHEMU MBALIMBALI ZA MWILI WAKE HADI KUPOTEZA FAHAMU  NA BABA YAKE MZAZI  ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA MARCO MBEMBELA (30) MKAZI WA SOGEA – TUNDUMA.
TUKIO HILO LILITOKEA TAREHE 19.03.2014 ALFAJIRI HUKO SOGEA KATA NA TARAFA YA TUNDUMA WILAYA YA MOMBA KWA TUHUMA KUWA ANATABIA YA  KUZURURA OVYO KATIKA NYUMBA ZA WATU.
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA WAZAZI/WALEZI KUTUMIA BUSARA KATIKA KUWAELEKEZA NA KUWAONYA WATOTO WAO BADALA YA KUWAPIGA KWANI NI HATARI KWA AFYA NA MAISHA YAO.
PIA HUKO WILAYA YA KYELA:
MTU MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA MATESO LAMSI (25) MKAZI WA KIJIJI CHA NDOBO ALIUAWA KWA KUPIGWA SEHEMU MBALIMBALI ZA MWILI WAKE NA KUNDI LA WANANCHI WALIOAMUA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI WAKITUMIA SILAHA ZA JADI FIMBO, MAWE NA MARUNGU.
TUKIO HILO LILITOKEA TAREHE 18.03.2014 SAA 20:00 USIKU KATIKA KIJIJI CHA NDOBO, KATA YA NDOBO, TARAFA YA NTEMBELA, WILAYA YA KYELA. CHANZO CHA TUKIO HILO NI TUHUMA ZA WIZI BAADA YA MAREHEMU KUKAMATWA AKIIBA KAKAO KWENYE SHAMBA LA JAPHET MWAKALINGA.
MAREHEMU ALIKUWA MHALIFU MZOEFU NA AMETOKA GEREZANI HIVI KARIBUNI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA TABIA YA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA BADALA YAKE WAWAFIKISHE WATUHUMIWA WANAO WAKAMATA KWA TUHUMA MBALIMBALI KATIKA MAMLAKA HUSIKA KWA HATUA ZAIDI ZA KISHERIA.
AIDHA KATIKA TUKIO JINGINE:
MTU MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA GODFREY KAYANGE (22) FUNDI MAGARI, MKAZI WA MAKAMBAKO ALIFARIKI DUNIA MUDA MFUPI WAKATI ANAPATIWA MATIBABU KATIKA HOSPITALI YA  WILAYA MBARALI BAADA YA KUGONGWA NA GARI LENYE NAMBA ZA USAJILI T.859 AGL/T.650 AKB AINA YA SCANIA TRUCK LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA DEREVA BENJAMIN MANDELE (38) MKAZI WA MAFINGA.
AJALI HIYO ILITOKEA TAREHE 19.03.2014 SAA 16:00 JIONI KATIKA KIJIJI CHA MKOMBE, KATA YA UBARUKU, TARAFA YA RUJEWA, WILAYA YA MBARALI MKOA WA MBEYA KATIKA BARABARA YA MBEYA/NJOMBE.
CHANZO CHA AJALI NI UZEMBE WA DEREVA KUTOKUMUONA MAREHEMU WAKATI AKIDANDIA GARI HILO NA KUMGONGA. MTUHUMIWA AMEKAMATWA NA GARI LIPO KITUO CHA POLISI RUJEWA. 
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO VYA MOTO HASA KWA KUZINGATIA SHERIA NA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA.
KATIKA MSAKO ULIOFANYIKA ENEO LA KASUMULU:
JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA RAIA WA PAKISTAN WATANO AMBAO NI 1. MOHAMED RASHID (35), 2. SADAM HUSSEIN (19), 3. NAWICED IGBILI (23), 4. GULU LAZA (31) NA 5. MUZZAFAR HAMED (24) WOTE WAKAZI WA NCHINI PAKISTAN  WAKIWA WAMEINGIA NCHINI BILA KIBALI.
WAHAMIAJI HAO HARAMU WALIKAMTWA TAREHE 18.03.2014 SAA 18:00 JIONI HUKO KATIKA ENEO LA KASUMULU, KATA YA NGANA, TARAFA YA UNYAKYUSA WILAYA YA KYELA.  WATUHUMIWA WAMEKABIDHIWA IDARA YA UHAMIAJI.
 KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII KUTOA TAARIFA ZA WATU WANAOWATILIA MASHAKA KATIKA MAENEO YAO ILI UCHUNGUZI ZAIDI UFANYWE DHIDI YAO.
Signed by:
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

TAZAMA JINSI VALENCIA ALIVYOUMIZWA VIBAYA CHINI YA JICHO

Antonio Valencia looked worse for wear after a nasty collision with Olympiacos forward Joel Campbell in the early stages of the Champions League second leg at Old Trafford.

The Manchester United winger went up for a header on the edge of the Olympiacos penalty with the on-loan Arsenal forward and came off second best.
He had to receive treatment from the United physios, and a large lump appeared next to his eye after the incident.
Ouch: Antonio Valencia was left with a lump above his eye after a nasty collision
Ouch: Antonio Valencia was left with a lump above his eye after a nasty collision

Bump: Valencia clashed heads with Joel Campbell in the early stages at Old Trafford
Bump: Valencia clashed heads with Joel Campbell in the early stages at Old Trafford
Impact: Valencia and Campbell clash heads on the edge of the Olympiacos penalty area
Impact: Valencia and Campbell clash heads on the edge of the Olympiacos penalty area



Fit to continue: The winger stayed on after consulting with the Manchester United physio
Fit to continue: The winger stayed on after consulting with the Manchester United physio


The Ecuador international was left out of the 3-0 defeat by Liverpool on Sunday, but returned to the line-up for the crucial second leg against their Greek opposition.
As a reward for his return to the starting XI, Valencia received a nasty eye lump.
Valencia was one of four changes to the United side against Liverpool. David Moyes also recalled Rio Ferdinand, Ryan Giggs and Danny Welbeck to the starting XI in a bid to overturn the 2-0 first-leg deficit.
Valencia was replaced by Ashley Young with 15 minutes remaining.

Seeing clearly? A huge lump starts to appear above Valencia's eye as he receives treatment
Seeing clearly? A huge lump starts to appear above Valencia's eye as he receives treatment

Brought down: The Ecuador international is tackled by Olympiacos' Alejandro Dominguez
Brought down: The Ecuador international is tackled by Olympiacos' Alejandro Dominguez
Under pressure: David Moyes made four changes to the team which lost 3-0 against Liverpool
Under pressure: David Moyes made four changes to the team which lost 3-0 against Liverpool

Vifusi vya ndege vyaonekana Australia?


John Young meneja mkuu wa halmasshauri ya usalama wa ndege nchini Australia
Waziri mkuu wa Australia amesema kuwa mitambo ya satelite ya nchi hiyo imenasa picha za vitu vinavyoonekana kama vifusi ambavyo huenda ni vya ndege ya Malaysia iliyopotea siku 13 zilizopita.
Waziri mkuu huyo, Tony Abbott, ameambia bunge mjini Canberra kwamba picha za Satelite zimeonyesha vitu viwili vinavyofanana na vifusi vya ndege hiyo.
Taarifa hii imejitokeza karibu wiki mbili baada ya ndege hiyo kutoweka na abiria zaidi ya miambili kutoka mjini Kuala Lumpur Malaysia kuelekea Beijing.
Msemaji wa halmashauri ya usalama wa safari za ndege, John Young, baadaye alisema kuwa vifaa hivyo ambavyo kimoja kina ukubwa wa mita 24, vimeonekana umbali wa kilomita 2500 kusini Magharibi mwa pwani ya Australia.
Aliongeza kwamba,vifusi itakuwa vigumu kuviona vifusi hivyo na pia huenda sio vya ndege hiyo.
Wakati taarifa hii ilipotolewa, kulikuwa na ndege ya Australia katika neo hilo , ndege zaidi zinatarajiwa kuwasili katika eneo lenyewe na pia manowari ya jeshi inaelekea huko.chanzo BBC

Wednesday 19 March 2014

BREAKING NEWS SONGEA DODOMA VIA MTERA KUANZA RASMI TAREHE 1/4/2014

Kwa mujibu wa taarifa toka kwa mkurugenzi Mkuu wa Super Feo Express kuanzia tarehe 1/4/2014 mabasi ya super feo yataanza rasmi safari ya Songea,Dodoma kupita Mtera na basi litakua likitoka songea saa 12:00asbh na kufika Dodoma saa 11:10 jioni  na kurudi songea katika muda kama huo na nauli itakua sh 38,500 tu za kitanzania KARIBU SUPER FEO EXPRESS

BREAKING NEWSSS!!!!!!!!!!! SONGEA TO DOM AND MBEYA TO DSM WITH SUPER FEO!


WAPENDWA WADAU WETU!
    TUNAYO FURAHA KUWATAARIFU KUWA LEO TUMEPOKEA KIBARI CHA MABASI YA SUPER FEO KUTEMBEA SONGEA DODOMA MUDA WETU NI KUTOKA SONGEA SAA 12:00ASBH NA KUFIKA DODOMA SAA 11:10 JIONI NA KURUDI HIVYO HIVYO NA MBEYA DSM TUTAENDELEA KUWAJUZA LINI DHAHABU INAANZA KUTEMBEA KATIKA NJIA HIZO!
        ASANTENI SANA
  SUPER FEO EXPRESS IN GOD WE TRUST

Yaliyojiri katika kesi ya Oscar Pistorius kumuua mpenzi wake

oscar-pistorius-6_2480644b
Mtaalamu wa mabomu aliyetoa ushahidi katika kesi inayomkabili Oscar Pistorius, alisema kuwa mwanariadha huyo hakuwa amevaa miguu yake bandia alipompiga risasi mpenzi wake Reeva Steenkamp nchini Afrika Kusini.
Ushahidi huu ulisikika katika kesi dhidi ya Pistorius inayoendelea Afrika Kusini.

Afisa huyo wa polisi alikuwa anatoa ushahidi wake kuhusu risasi zilizomuua marehemu Reeva Steenkamp.

Bwana Pistorius amekana madai ya kumuua mpenzi wake kwa maksudi wakati wa siku ya Valentine’s Day mwaka 2013 akisema kuwa alidhani alikuwa jambazi aliyekuwa amevamia nyumba yake.
Upande wa mashitaka unasema kuwa Oscar alimuua mpenzi wake kwa maksudi.
Katika siku ya 13 ya kesi hiyo, Kapteni Christian Mangena alisema kuwa, tathmini ya eneo ambapo mauaji yalifanyika, ilionyesha kwamba bwana Pistorius hakuwa amevalia miguu yake bandia alipompiga risasi Reeva.
Duru zinasema kuwa ni muhimu kujua ikiwa Pistorius alivalia miguu yake bandia au kwa sababu itasaidia upande wa utetezi kuonyesha kuwa mauaji hayo hayakuwa ya kupangwa.
Kapteni Mangena pia alisema kuwa japo hakuweza kubaini umbali alikokuwa Pistorius alipofyatua bunduki yake, hakuwa mbali na mita tatu kutoka katika bafu yake.
Inaarifiwa ushahidi huu unaambatana na utetezi wa Pistorius aliyesema kuwa alifyatua bunduki yake alipokuwa akisimama karibu na mlango wa bafu lake.
Alisema kuwa Reeva alianguka kabla ya risasi nyingine mbili kumgonga mkononi mwake na kichwani.
SOURCE: BB

Qatar wakanusha kununua nafasi ya kuandaa kombe la dunia 2022

SeppHammam_468x606-95027
Kamati ya maandalizi ya michuano ya Kombe la dunia nchini Qatar mwaka 2022 imetetea Uhalali wa mkataba wake wa kuandaa michuano ya kombe la dunia baada ya Gazeti moja kudai kuwa lina mashaka na mchakato wa maandalizi unavyoendelea.
Aliyekuwa makamu wa Rais wa Fifa, Jack Warner na familia yake walilipwa zaidi ya Pauni milioni 1 na Kampuni inayomilikiwa na Afisa wa zamani wa mchezo wa mpira wa miguu kutoka nchini Qatar, Gazeti la Daily Telegraph limeripoti madai hayo.
Lakini kamati ya maandalizi ya kombe la dunia nchini Qatar imesema mkataba uliopata ulifuata sheria za Fifa na kuwa haikua ikifahamu shutuma zozote zinazohuzu makubaliano ya kibiashara baina ya watu hao wawili.
Gazeti hilo limedai kuwa Warner na Watoto wake wamelipwa kiasi hicho cha fedha na kampuni inayomilikiwa na Mohamed Bin Hammam.
Baadhi ya malipo yanadaiwa kufanyika muda mfupi baada ya Qatar kushinda haki ya kuhodhi mashindano ya Kombe la dunia mwaka 2022.
Bin Hammam alikuwa mtu mwenye nguvu kubwa ndani ya Fifa kwa miaka mingi lakini alipewa adhabu ya kufungiwa maisha kushiriki maswala yahusuyo shirikisho hilo baada ya kushutumiwa kuwa na maslahi binafsi alipokuwa Kiongozi wa shirikisho la soka barani Asia.
Nyaraka ambazo gazeti la Telegraph limedai kuziona, huenda zikazua maswali mengi kutoka kwa Mkuu wa uchunguzi wa maswala ya maadili ndani ya Fifa, Michael Garcia, ambaye anachunguza namna gani ambavyo haki za maandalizi ya michuano hiyo zilipatikana kwa ajili ya mwaka 2018 na 2022.
katika taarifa yao, Waandaaji wa michuano hayo nchini Qatar wamesema haki ya kuandaa michuano hiyo ilifuata taratibu zote za Fifa na kufuata maadili yote.
Warner na Bin Hammam walikataa kutoa kauli juu ya madai yaliyotolewa dhidi yao walipoulizwa na BBC kuhusu tuhuma kutoka gazeti la the Daily Telegraph.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHITIMISHA SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA WIKI YA MAJI KITAIFA WILAYANI MPWAMPWA MKOA WA DODOMA LEO

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimtwisha ndoo ya maji Bi. Amina Rajab, mkazi wa Wilayani Mpwapwa, baada ya kuzindua rasmi Kisima cha Bomba la maji, wakati wa sherehe za maadhimisho ya Wiki ya maji zilizofanyika Kitaifa Wilaya ya Mpwapwa Mkoani Dodoma leo, Machi 19, 2014. 
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja wa Mradi wa Maji wa Wilaya ya Mpwapwa, Shadrack Matemba (wa pili kulia) wakati alipotembelea moja ya chanzo cha maji wakati wa sherehe za maadhimisho ya Wiki ya maji zilizofanyika Kitaifa Wilaya ya Mpwapwa Mkoani Dodoma leo, Machi 19, 2014. Kulia kwa Makamu ni Mama Asha Bilal na Waziri wa Maji , Profesa Jumanne Maghembe. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka jiwe la msingi kuashiria kuzindua rasmi Kisima cha Bomba la maji sikiliza wakati wa sherehe za maadhimisho ya Wiki ya maji zilizofanyika Kitaifa Wilaya ya Mpwapwa Mkoani Dodoma leo, Machi 19, 2014. Kushoto kwa Makamu ni Waziri wa Maji , Profesa Jumanne Maghembe,(kushoto) ni Mama Asha Bilal
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifurahia ngoma ya asili ya kabila la Wagogo wakati alipokuwa akiwasili katika sherehe za maadhimisho ya Wiki ya Maji zilizofanyika Kitaifa Wilaya ya Mpwapwa Mkoani Dodoma leo, Machi 19, 2014.
 Baadhi ya wananchi wa Wilayani Mpwapwa wakimsikiliza Makamu wa Rais wakati akiwahutubia.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Rehema Nchimbi, wakati wa sherehe za maadhimisho ya Wiki ya maji zilizofanyika Kitaifa Wilaya ya Mpwapwa Mkoani Dodoma leo, Machi 19, 2014.Picha na OMR

MATUKIO YA BUNGE LA KATIBA LEO




Mjumbe wa Bunge Maalum, Evod Mmanda akifafanua kanuni za bunge hilo leo mjini Dodoma.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda (kulia) akizungumza na Mjumbe wa Bunge wa Maalum ambaye pia ni Spika wa Baraza la wawakilishi Zanzibar, Pandu Ameir Kificho wakati wa semina ya kuhusu kanuni za bunge hilo leo mjini Dodoma.
Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ally Iddi  akijadiliana jambo na Waziri Mkuu Mizengo Pinda(kushoto) wakati wa semina ya kuhusu kanuni za bunge hilo leo mjini Dodoma.
Waziri wa Katiba na Sheria ,Dk. Rose Asha Migiro akijadiliana jambo na Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia ,Januari Makamba wakati wa semina ya kuhusu kanuni za bunge hilo leo mjini Dodoma.

Mjumbe wa Bunge Maalum Dk.  Tulie Akson  akifafanua kanuni za bunge hilo leo mjini Dodoma

LIVE MATCH CENTRE:::YANGA 1 VS AZAM 0

 KIKOSI CHA YANGA - NGASSA AANZIA BENCHI

1. Juma Kaseja - 29
2. Juma Abdul - 12
3. Oscar Joshua - 4
4. Nadir Haroub "Cannavaro" - 23
5. Kelvin Yondani - 5
6. Frank Domayo - 18
7. Saimon Msuva - 27
8. Hassan Dilunga - 26
9. Didier Kavumbagu - 7
10. Hamisi Kizza - 20
11. Emmanuel Okwi - 25
Subs:
1. Barthez, 2.Luhende, 3. Chuji, 4.Nizar, 5. Javu, 6. Tegete, 7. Ngasa

KIKOSI CHA AZAM FC

Aishi, Nyoni, Michael, Morad, Balou, Himid, Sure Boy, Bocco, Kipre Tchetche na Mcha

DK 5'...Azam 0 Yanga 0 
DK 10 Bocco aliumia akalala chini, amerejea uwanjani. 
14' kavumbagu anaipatia yanga goli la kuongoza.....azam 0 yanga 1 

20' azam wanapata bao ila refa analikataa...kipre alifanya madhambi kabla ya kufunga.
21' kipre anapiga shuti linagonga mwamba..Azam wanashambulia kwa kasi sasa

24' erasto nyoni anapata kadi ya njano, kamkwatua okwi.

Dakika ya 30, Young Africans 1 - 0 Azam FC 
DK 37 David Mwantika anamchezea rafu Owki kwenye box ila refa anapeta, kwa maoni yangu yanga wamenyimwa penalty ya waziwazi
Dakika ya 43 ya kipindi cha kwanza: Yanga 1, Azam 0 
Mapumziko: Yanga 1-0 Azam 
mpira unachelewa kuanza, nyavu za goli la kaskazini zinamatatizo. wachezaji wanapasha misuli wakisubiri 

Ahukumiwa kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kupatikana na hatia ya kunyanyasa na kumtesa mtoto.

MWANAMKE Mwanahawa Nassoro(32) Mkazi wa Mtaa wa Airport jijini Mbeya amehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kupatikana na hatia ya kunyanyasa na kumtesa mtoto.


Baba mzazi wa mtoto John akiwa amekaa na mwanae mara tu baada ya hukumu kutolewa
MWANAMKE Mwanahawa Nassoro(32) Mkazi wa Mtaa wa Airport jijini Mbeya amehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kupatikana na hatia ya kunyanyasa na kumtesa mtoto.

Mwanamke huyo alipandishwa katika Mahakama ya Mwanzo ya Mbeya mjini juzi kutokana na kosa lililokuwa likimkabili la  kumtesa mtoto John Paul(03) ambaye ni mtoto wa kaka yake.

Akisoma mashitaka mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Mbeya mjini, Salome Mwakyosi, mwendesha mashitaka wa Polisi  Kopro Anthon alisema mtuhumiwa alitenda kosa hilo Machi 12, Mwaka huu kwa nyakati tofauti kwa kumfungia ndani na kumnyima chakula kinyume cha sheria namba 241 ya makosa ya jinai sura ya 16 ya kanuni ya adhabu iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Alisema Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Airport, Rehema Mohammed ndiye aliyebaini na kutoa taarifa kwenye uongozi wa Mtaa ambapo mtuhumiwa alikamatwa na hatimaye kufikishwa katika kituo cha Polisi kwa ajili ya hutua za kisheria.

Upande wa Mashitaka ulikuwa na mashahidi wane, ambapo  wawili kati yao ndiyo waliotoa ushahidi ambao ni pamoja na Mjumbe wa Serikali ya Mtaa na Mtoto aliyefanyiwa ukatili huo ambaye alimtambua mahakamani Shangazi yake Mwanahawa licha ya kuwepo watu wengi.

Mtoto huyo alifika mahakamani kutoa ushahidi baada ya afya yake kuimarika kutokana na kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

 Hakimu alipomuuliza mtoto kuhusu mtu aliyekuwa akimpiga alimuonesha Mwanahawa mara tatu ambapo alizidi kumuonesha Shangaza yake huyo.

Kwa upande wake mtuhumiwa wa kesi hiyo alipoulizwa kuhusiana na kosa hilo alikiri ambapo Hakimu aliridhika na ushahidi uliotolewa na pande zote mbili ikiwa ni pamoja na kukiri kwa mtuhumiwa.

Kutokana na ushahidi huo Mahakama hiyo na ilimtia hatiani mshitakiwa kwa kumuadhibu kutumikia  kifungo cha miaka mitatu jela ili iwe fundisho kwa watu wanaofanya vitendo vya kikatili dhidi ya watoto

WAZEE WA KLABU YA YANGA WASITISHA MAANDAMANO YAO


Baraza la wazee wa Klabu ya Yanga, leo limetoa tamko la kusitisha maandamano yao ambayo walikuwa wameyapanga kufanyika ili kushinikiza serikali kutoa kibali cha Ujenzi wa uwanja wao wa kisasa unaotarajia kujengwa sehemu ya Jangwani, Dar es Salaam.

Tamko hilo la kusitisha maandamano hayo limetoleo mara baada ya baadhi ya viongozi wa juu wa timu hiyo kukutana na viongozi wa serikali.
Viongozi hao wa serikali walitoa tamko kuhusu kushughulikia ombi lao hali iliyosababisha viongozi wa Yanga kusitisha maandamano yao waliyokuwa wameyapanga kuyafanya juma hili.

Juma lililopita Katibu wa baraza hilo, Ibrahim Akilimali alitoa siku tano kwa Baraza la Madiwani Manispaa ya Ilala, liwe limewapa kibali cha ujenzi huo, vinginevyo waliahidi kufanya maandamano makubwa.

Amesema  viongozi wa juu wa klabu hiyo walikutana na viongozi wa serikali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sadik Mecky Sadik, Meya wa Ilala Jery Silaa na Diwani wa Kata ya Jangwani ambapo walikubaliana ombi lao kufanyiwa kazi.
Akilimali amesema serikali kupitia Manispaa ya Ilala ilieleza kuwa ombi lao linashughulikiwa kwa haraka, hivyo aliwataka wanachama wa klabu hiyo kuelewa jambo hilo bila kuwepo na migogoro.

Ameweka wazi kuwa wanaamini serikali kupitia Manspaa ya Ilala watalishughulikia ombi lao, ingawa amesisitiza kuwa ikitokea ombi lao hilo linaloshughulikiwa likija na majibu ya “hapana” watatafuta mbinu nyingine.

"Sisi tumeomba hivyo majibu ni mawili ndiyo tumepata au tumekosa, ikitokea likaja jibu la kukosa hapo ndiyo kutakuwa na utata na kuamua cha kufanya," alisema katibu huyo wa baraza la wazee wa klabu ya Yanga.
 
Ameongezea kuwa klabu hiyo imejiandaa kuwalipa watu waliongezeka katika eneo lao, hivyo hawaoni sababu za kwenda kujenga nje ya mji wakati wao ni watoto wa mjini.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAR 19.03.2014 VICHWA VIKUBWA WARIOBA AFUNIKA,MAHABUSU AJINYONGA KITUONI NA PONDA SASA NJIA PANDA.