Mkazi wa Kijiji cha Kihinga, Kata ya Bugarama wilayani Ngara mkoani 
Kagera(jina tunalo), anashikiliwa katika kituo kidogo cha polisi cha 
kata hiyo baada ya kutuhumiwa kuuza kilo moja ya nyama ya binadamu kwa 
Sh100,000.
Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kihinga, Hassan Mohamed alisema 
kuwa jana saa mbili usiku, wananchi walipeleka fedha nyumbani kwake 
kununua nyama hiyo na alipowaona alikimbia na wananchi hao kwa hasira 
walimkimbiza ili kumuua na hapo hapo kuunguza nyumba yake.
“Mgambo ndio walimnusuru asiuawe na wananchi wenye hasira kali na 
alikimbizwa kituo kidogo cha polisi Kata ya Bugarama ili kuokoa maisha 
yake “.
Akizungumza na gazeti hili, Kamanda wa mgambo wa kijiji hicho, 
Emanuel Kaloli alisema wananchi waliandamana baada ya kusikia taarifa za
 kuwapo mtu anayeuza nyama ya binadamu na kutaka kuhakikisha ukweli huo.
Alisema baada ya wananchi kufika, walianza kumshambulia na kutaka 
kumuua, lakini wanamgambo wa kitongoji walifika kisha kumuokoa mtuhumiwa
 na hatimaye kumfikisha kituo cha polisi kwa ajili ya usalama wake.
“Kijana aliyefahamika kwa jina la Man Balyamwabo mkazi wa Shina la 
Kalenge katika kitongoji hicho, ndiye aliyeambiwa kuwa angeuziwa nyama 
hiyo ya binadamu na kuleta taarifa katika uongozi wa kijiji ili uweze 
kuchukua hatua zaidia”.Alisema Kaloli.
Alisema nyumba aliyounguziwa pamoja na mali iliyokuwamo ndani hasa 
maharage, mavazi na vitu vinginevyo inakadiriwa kuwa na thamani ya 
Sh2.6milioni. Pamoja na kuwepo kwa tukio hilo, baadhi ya wananchi 
walisema mtuhumiwa inasemekana ni raia wa nchi jirani ya Burundi na 
alianza kuishi katika kitongoji hicho tangu mwaka 1981 kama kibarua wa 
kilimo kwenye mashamba.
Taarifa zinasema kuwa katika kuishi kwake na ndugu yake aliyefahamika
 kwa jina la Kahungu walikuwa wakituhumiana kwa uchawi na ilifikia 
mahala wakatofautiana na kaka yake ambaye alirejea kwao.
Polisi wilayani Ngara imethibitisha kumpokea mtuhumiwa huyo na kwamba
 linafanya mahojiano ya kina kwa kushirikiana na viongozi wa kijiji ili 
kubaini ukweli wa tukio hilo

 
No comments:
Post a Comment