Saturday 13 December 2014

Matokeo ya Simba vs Yanga

Screen Shot 2014-12-13 at 7.09.29 PM
Timu ya Simba imeibuka na ushindi baada ya kuichapa timu ya Yanga 2-0 huku timu ya Yanga wakiambulia kuondoka na maumivu ya kushindwa kufurukuta kwa bao hata moja.
Wafungaji wa magoli kutoka timu ya Simba ni Awadh Juma na Elias Maguri ambapo mabao yote yamefungwa katika kipindi cha kwanza.
Kwa mara ya pili tena timu ya SIMBA wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa Nani Mtani Jembe baada ya kutwaa ubingwa huo mwaka jana walipoichapa Yanga bao 3 -1.
Kwa upande wa zawadi Simba wamefanikiwa kutwaa milioni 92 huku Yanga wakiondoka milioni 7.
 Wachezaji wa timu ya Simba wakishangilia bao la pili lililofungwa na Elias Maguli katika dakika ya 40 ya kipindi cha kwanza. Mabao yote ya Simba yamefungwa katika kipindi cha kwanza huku bao la kwanza likifungwa na Awadh Juma katika dakika ya 30.
 Mashabiki wa Simba wakishangilia moja ya mabao yaliyofungwa na timu yao.
 Andreu Coutihno, akimiliki mpira katikati ya mabeki wa Simba…
Mchezaji mpya wa Yanga, kutoka nchini Liberia, Kpah Sherman. akisomba kijiji cha mabeki wa Simba…. Hadi mpira unaisha jumla ya mashabiki wasiopungua wanne wa Yanga walikuwa wameshazimia uwanjani. 
Mashabiki wa Simba waliojaza kwenye dimba la uwanja wa taifa

Umati wa wana jangwani leo taifa

Road Rage

 http://xmediaeco.files.wordpress.com/2010/11/australian_slippery_road_surface_sign.png



Take the Test — Do You Have Road Rage?

Aggressive driving habits can threaten your safety, the safety of your passengers and others driving on the road. Many people experience some level of road rage while they travel on the road. Dealing with road rage and aggressive drivers involves patience and the ability to remain calm.
See where you stand with road rage — take the quiz now.

 http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/01408/signs_1408319c.jpg

 Yes or No, Do You ...

  1. Overtake other vehicles only on the left?
  2. Avoid blocking passing lanes?
  3. Yield to faster traffic by moving to the right?
  4. Keep to the right as much as possible on narrow streets and at intersections?
  5. Maintain appropriate distance when following other motorists, bicyclists, motorcyclists, etc.?
  6. Provide appropriate distance when cutting in after passing vehicles?
  7. Use headlights in cloudy, rainy, and other low light conditions?
  8. Yield to pedestrians?
  9. Come to a complete stop at stop signs, before right turn on red, etc.?
  10. Stop for red traffic lights?
  11. Approach intersections and pedestrians at slow speeds to show your intention and ability to stop?
  12. Follow right-of-way rules at four-way stops?
  13. Drive below posted speed limits when conditions warrant?
  14. Drive at slower speeds in construction zones?
  15. Maintain speeds appropriate for conditions?
  16. Use vehicle turn signals for all turns and lane changes?
  17. Make eye contact and signal intentions where needed?
  18. Acknowledge intentions of others?
  19. Use your horn sparingly around pedestrians, at night, around hospitals, etc.?
  20. Avoid unnecessary use of highbeam headlights?
  21. Yield and move to the right for emergency vehicles?
  22. Refrain from flashing headlights to signal a desire to pass?
  23. Drive trucks at posted speeds, in the proper lanes, using non-aggressive lane changing?
  24. Make slow, deliberate U-turns?
  25. Maintain proper speeds around roadway crashes?
  26. Avoid returning inappropriate gestures?
  27. Avoid challenging other drivers?
  28. Try to get out of the way of aggressive drivers?
  29. Refrain from momentarily using High Occupancy Vehicle (HOV) lanes to pass vehicles?
  30. Focus on driving and avoid distracting activities (e.g., smoking, use of a car telephone, reading, shaving)?
  31. Avoid driving when drowsy?
  32. Avoid blocking the right-hand turn lane?
  33. Avoid taking more than one parking space?
  34. Avoid parking in a disabled space (if you are not disabled)?
  35. Avoid letting your door hit the car parked next to you?
  36. Avoid stopping in the road to talk with a pedestrian or other driver?
  37. Avoid inflicting loud music on neighboring cars?

Score Yourself...

Are you an Aggressive Driver or a Smooth Operator? Answering "No" to more questions means you're a more aggressive driver.
Number of "No" Answers How You Rate as a Driver
1-3 Excellent
4-7 Good
8-11 Fair
12+ Poor

Driving Safety

Safe driving is a priority so make sure that you follow these tips if you need to make phone calls whilst driving.

  1. Keep your phone on Voicemail when driving.
  2. If you really must make or receive calls, always use a hands-free kit.
  3. Make sure you inform the person you are speaking to that you are driving so they understand that you need to concentrate.
  4. If possible tell the person that you will call back when you have parked safely.
  5. Avoid long, complex or emotional conversations.
  6. If you have a speed dial function on your phone, use this to enter frequently-called numbers. One touch dialing is much safer than dialing manually.
  7. Do not take notes or look up phone numbers while driving.
  8. Don’t accept or make calls if traffic and weather conditions would make it unsafe to do so.
 Safety Tips
  • Get to know your cell phone and its features, such as speed dial and redial.
    Carefully read your instruction manual and learn to take advantage of valuable features most cell phones offer, including automatic redial and memory. Also, work to memorize the phone keypad so you can use the speed dial function without taking your attention off the road.
  • When available, use a hands-free device.
    A number of hands-free cell phone accessories are readily available today. Whether you choose an installed mounted device for your cell phone or a speaker phone accessory, take advantage of these devices if available to you.
  • Position your cell phone within easy reach.
    Place your cell phone within easy reach and where you can grab it without taking your eyes off of the road. If you receive a call at an inconvenient time, if possible, let your voice mail answer it for you.
  • Suspend conversations during hazardous driving conditions or situations.
    Let the person you are speaking with know you are driving. If necessary, suspend the call in heavy traffic or hazardous weather conditions. Rain, sleet, snow and ice can be hazardous, but heavy traffic can be just as dangerous. As a driver, your first responsibility is to pay attention to the road.
  • Do not take notes or look up phone numbers while driving.
    If you are reading an address book or business card, or writing a "to do" list while driving a car, you are not watching where you are going. It's common sense. Don't get caught in a dangerous situation because you're reading or writing and not paying attention to the road or nearby vehicles.
  • Dial sensibly and assess the traffic. If possible, place calls when you are not moving or before pulling into traffic.
    Try to plan your calls before you begin your trip, or attempt to coincide your calls with times you may be stopped, such as at a stop sign, red light or in a parking space. But, if you need to dial while driving, follow this simple tip: Dial only a few numbers, check the road and your mirrors, then continue dialing.
  • Do not engage in stressful or emotional conversations that may be distracting.
    Stressful or emotional conversations and driving do not mix — they are distracting and even dangerous when you're behind the wheel of a car. Make people you are talking with aware you are driving and, if necessary, suspend conversations which have the potential to divert your attention from the road.
  • Use your cell phone to call for help.
    Your cell phone is one of the greatest tools you can own to protect yourself and your family in dangerous situations — with your phone at your side, help is only three numbers away. Dial 911 or another local emergency number in emergencies such as a fire, traffic accident, road hazard or medical emergency. Remember, an emergency call is a free call on your cell phone!
  • Use your cell phone to help others in emergencies.
    Your cell phone provides the opportunity to be a "Good Samaritan" in your community. If you see a car accident, crime in progress or other serious emergency where lives are in danger, call 911 or another local emergency number, as you would want others to do for you.
  • Call roadside assistance or a special cell non-emergency assistance number when necessary.
    Certain situations you encounter while driving may require attention, but are not urgent enough to merit a call for emergency services. Even so, you still can use your cell phone to lend a hand. If you see a disabled vehicle posing no serious hazard, a broken traffic signal, a minor traffic accident where no one appears injured or a vehicle you know is stolen, call roadside assistance or another special non-emergency cell number

Mayweather kuchapana na Pacquiao Mei 2


Mayweather akipigana.Bondia huyo amesema kuwa yuko tayari kutetea taji lkake dhidi ya Manny Pacquiao mwaka ujao. 


Bondia Floyd Mayweather ametaja tarehe 2 mwezi May mwaka 2015 kama siku ya pigano kati yake na Manny Pacquiao .
Kulingana na gazeti la Daily mail nchini Uingereza ,uvumi kwamba pigano hilo ambalo litakuwa la kiwango kikubwa cha malipo kuwahi kutokea katika historia ya ndondi ulianza pale Pacquiao alipoonyesha mchezo mzuri kati yake na Chris Algieri mjini Macau wiki mbili zilizopita.
Na sasa Maywheather kupitia kampuni yake moja ya mauzo amesema kuwa yuko tayari kupambana na Pacman katika pigano lake linalokuja.
 

Bondia Manny Pacquiao Kushoto akimchapa Tim Bradley katika mojwapo ya mapigano yao.
Bondia huyo ambaye ndiye mwanamichezo tajiri duniani amesema kuwa mashabiki wa ndondi wamesubiri sana pigano hilo na sasa yuko tayari.
''Kizuizi kikubwa cha pigano hilo ni promota wa Pacquiao Bob Arum ,lakini najua kwamba sisi sote tunalihitaji pigano hili'',alisema Mayweather.. Kwa hivyo ni wakati lifanyike.
Mayweather alikiri kwa mara ya kwanza majadiliano yanaendelea kwa siri na kuongeza kwamba hamuogopi mtu yeyote.''Miaka iliopita tulikuwa na tatizo la kupimwa mikojo na damu,swala ambalo Pacman amekuwa akilipinga''.aliongezea Mayweather.

 

Bondia Mayweather baada ya kushinda katika baadhi ya mapigano yake.
Hatahivyo upande wa Mayweather ni vile kitita cha pigano hilo kitakavyogawanywa.
Inakadiriwa kuwa pigano hilo litagharimu dola millioni 300.
Upande wa Pacman tayari umekubali fedha hizo kugawanywa kwa 60-40 huku Mayweather akichukua kitita kikubwa,ijapokuwa kuna madai kwamba Mayweather huenda akadai asilimia kubwa zaidi iwapo makubaliano yataafikiwa

Roy Keane adaiwa alizua migogoro Villa

 

Aliyekuwa naibu mkufunzi wa kilabu ya Aston Villa Roy Keane
  
Naibu Kocha wa Kilabu ya Aston Villa Roy Keane na mshambuliaji Gabriel Agbonlahor nusra wapigane wakati wa mazoezi katika majibizano ya manane yaliomlazimu kocha huyo kuondoka katika kilabu hiyo.
Kulingana na gazeti la Daily mail nchini Uingereza,Roy Keane mara kwa mara alihusika katika mgogoro na wachezaji wa muhimu wa kilabu hiyo miezi sita tu baada ya kujiunga na kilabu hiyo.
Inadaiwa kuwa hali ya mazingira wakati wa mazoezi ilibadilika mara kwa mara wakati wa kuwasili kwa Roy Keane.
Kulikuwa na hali ya wasiwasi wakati kocha huyo alipozozana na nahodha wa kilabu hiyo Agbonlahor mbele ya wachezaji wenzake wakati wa mazoezi kabla ya naibu huyo kuondoka katika timu hiyo.


                      Nahodha wa kilabu ya Aston Villa Agbonlahor akielekea kufunga bao

Inadaiwa kuwa Agbonlahor alikuwa akijadiliana na mkufunzi wa timu hiyo Lambert wakati Keane alipoingilia kati.
Lakini Agbonlahor alikataa kunyamaza na badala yake akamwambia Keane kwamba anazungumza na kocha.
Wawili hao baadaye walihusika katika majibizano na ilibidi watawanywe.
Uhasama huo uliendelea kati ya wawili hao ndiposa Lambert akafanya kikao na Roy Keane wakati ilipoamuliwa kwamba nahodha huyo wa kitambo wa timu ya Manchester United ataondoka katika kilabu hiyo

Mkutano wa mazingira wa UN warefushwa

 Waziri wa mazingira wa Peru akihutubia mkutano mjini Lima 
Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu mazingira ambao ulikuwa umalizike mapema, unaendelea nchini Peru kwa siku ya 13 huku wajumbe wakijaribu kufikia makubaliano kuhusu namna ya kupambana na kuzidi kwa joto duniani.

Wamekwama katika hoja kuhusu ahadi ambazo zinaweza kutolewa na nchi zilizoendelea na zinazoendelea.
Mataifa yanayoharibu mazingira zaidi, kama Marekani na ya Umoja wa Ulaya, yanataka kutangaza mwaka ujao yatapunguza gesi inayozidisha joto kwa kiasi gani.
Lakini piya yanataka nchi nyengine zaidi zitoe ahadi kama hiyo.
Nchi kuu zinazoendelea, pamoja na India na Uchina, zinapinga hayo huku nchi maskini zaidi zinataka msaada zaidi wa fedha ili kupambana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa.

Hofu ya TZ kunyimwa msaada na Marekani

Mbunge Zito Kabwe mwenyekiti wa kamati iliyowasilisha ripoti kuhusu sakata ya Escrow 
 
Serikali ya Tanzania iko hatarini kukosa dola za Marekani milioni mia saba sawa na trilioni 1.1 kwa fedha za Tanzania kwa ajili ya mradi wa pili wa mfuko wa changamoto za Milenia (MCC) kutokana na kushamiri kwa vitendo vya rushwa nchini humo.
Marekani imebainisha kuwa mkataba wa pili wa miradi inayofadhiliwa na shirika lake la Changamoto za Milenia (MCC) utategemea hatua zitakazochukuliwa na serikali ya Tanzania dhidi ya wahusika wa kashfa hiyo.
Haya yanajiri wakati Rais Jakaya Kikwete akisubiriwa kutoa maamuzi ya mapendekezo yaliyofikiwa na Bunge kuhusiana na sakata la uchotwaji fedha zaidi ya Sh. bilioni 300 kutoka kaunti ya Tegeta Escrow wiki ijayo.
Katika tamko hilo kwa umma ambalo limewekwa kwenye tovuti ya MCC, bodi ilieleza kutambua umuhimu wa kusubiri na kuona utekelezaji kamilifu wa tamko lililotolewa na Ikulu ya Tanzania Desemba 9, mwaka huu kwamba itachukua hatua za haraka na kutoa maamuzi dhahiri na thabiti kuhusu maazimio ya Bunge juu la suala la IPTL.
Taarifa iliyotolewa na Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania ilieleza kuwa wakurugenzi wa MCC waliokutana katika mkutano wao uliofanyika Desemba 10, mwaka huu wamesikitishwa na hali ya rushwa nchini Tanzania.
 
Bunge la Tanzania kikaoni
Uamuzi huo wa Marekani ambayo inafadhili miradi mingi ya mabilioni ya fedha ni mtihani wa pili kwa Rais Kikwete baada ya ule wa maazimio ya Bunge yaliyotaka viongozi wakiwamo mawaziri waliotajwa katika kashfa hiyo kuwajibishwa.
Wanaotakiwa kuwajibishwa na Rais Kikwete ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa, Sospeter Muhongo na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka.
Wengine ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakimu Maswi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema.
Novemba mwaka huu, Serikali ya Marekani kwa kupitia MCC, ilikubali kutoa ruzuku ya hadi Dola za Kimarekani milioni 9.78 kwa ajili ya maandalizi ya miradi ya uwekezaji yenye matokeo makubwa katika sekta ya nishati nchini.
Tanzania ilikuwa mojawapo ya nchi kumi zilizojadiliwa na Bodi ya MCC iliyokutana kuangalia kama nchi hizo zimekidhi vigezo vya kuendelea na mchakato wa kuandaa mikataba mipya.
Wakati wa mkutano wa 16 na 17 wa Bunge, Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi), alidokeza kusudio la Marekani kukataa kutoa fedha kwa ajili ya miradi ya MCC, lakini Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alikanusha taarifa hizo.
Juhudi za BBC kumtafuta Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mark Childress,aweze kuzungumzia juu ya ripoti hiyo ziligonga mwamba kutokana na sababu za kiprotokali.

Bensouda kusitisha uchunguzi Darfur

 

Moreno Ocampo alyekuwa kiongozi wa mashtaka wa ICC na kiongozi wa sasa wa mahakama hiyo Fatou bensoud. 
Mwendesha mashtaka mkuu kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita Fatou Bensouda amesema kuwa atasitisha uchunguzi kuhusu uhalifu wa kivita ulioendeshwa katika eneo la Darfur nchini Sudan kutokana na ukosefu wa usaidizi kutoka kwa baraza la usalama la umoja wa mataifa.
Kwenye taarifa yake kwa baraza hilo mwendesha mashtaka huyo amesema kuwa wanawake na wasichana wanaendelea kuathirika zaidi katika jimbo hilo.

 

Rais wa Sudan Omar El Bashir anayetafutwa na mahakama ya ICC kwa kuhusishwa na uhalifu dhidi ya binaadamu katika eneo la Darfur.
 
Amesema kuwa kutokuwepo kwa hatua zozote kutoka kwa baraza la umoja wa mataifa kumechangia kuendelea kwa uhalifu na sasa amelazimika kutumia raslimali za mahakama hiyo kwa masuala mengine.
Mwaka 2009 mahakama ya ICC ilimhusisha rais wa Sudan Omar al-Bashir na uhalifu wa kivita kwenye jimbo la Darfur lakini hadi sasa hajakamatwa wala hata mmoja wa washirika wake.