Friday 14 February 2014

SUMAYE : ASEMA HAKUNA UTAWALA BORA WENYE UCHUMI DHAIFU

WAZIRI mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, amesema mahali popote penye uchumi dhaifu hata utawala bora hauwezi kupatikana mahali hapo.


Akizungumza na jumuiya ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu jijini Mwanza, katika kongamano lililoandaliwa na serikali ya wanafunzi wa Chuo cha Biashara (COBESO) Mwanza jana katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Chama cha Ushirika Nyanza, Sumaye alisema uchumi dhaifu huweza hata kuhatarisha usalama wa nchi kwa kuwa ni rahisi sana kusababisha mifarakano ndani ya jamii, kwa sababu jinsi watu wanavyokuwa na maisha magumu, ndivyo wanavyokuwa hawaridhiki.

Kwa mujibu wa Sumaye, uchumi dhaifu huweza kusababisha hasira za muda wote za wananchi dhidi ya serikali yao au hata baina yao wenyewe kwa wenyewe, na hasa panapokuwa na tofauti kubwa ya hali za maisha.

No comments: