Monday 24 February 2014

DKT. MAGUFULI ATEMBELEA ENEO ILIPOTOKEA AJALI YA MAGARI YALIYOTEKETEA KWA MOTO MIKESE, MOROGORO LEO

Dkt. Magufuli akiangalia hali ya lori hilo mara baada ya kuwasili katika eneo la tukio, Mikese Morogoro.
Dkt. Magufuli akiongea na baadhi ya wahanga wa ajali hiyo.
Kwa Hisani ya Michuzi Blog
Waziri wa Ujenzi,Dkt. John Pombe Magufuli amesafiri akitokea Mkoani Dodoma anakohudhuria Vikao vya Bunge la Katiba na kwenda moja kwa moja Morogoro maeneo ya Mikese (Kilomita kumi kutoka Mzani wa Mikese kuelekea Dar), ambapo magari mawili yaligongana na kuteketea kwa moto na kusababisha kifo cha mtu mmoja alietambulika kwa jina la Moud Amin.

Ajali hiyo ambayo imetokea mapema leo ilifunga barabara yote ya Dar - Morogoro, takribani kwa masaa zaidi ya mawili na kusababisha foleni kubwa ya takribani kilomita 30. Malori hayo, lori moja lilikuwa likitokea Bukoba, mkoani Kagera likielekea Dar na lori lingine likielekea Sumbawanga, mkoani Rukwa. Chanzo cha ajali bado hakijafahamina na uchunguzi bado unaendelea.

Aidha, Dkt. Magufuli kwa mamlaka aliyopewa, ameruhusu malori yaliyokuwa yamesongamana kupita mzani wa Mikese bila kupimwa ili kuondoa usumbufu mwingine katika mzani wa Mikese.

Dkt. Magufuli kwa pamoja na mhandisi wa mkoa wa Morogoro Mhandisi Tenga walisimamia ukwamuaji wa malori hayo.

No comments: