Monday 24 February 2014

Hatimaye Hati yatolewa Rais wa Ukraine anatafutwa Akamatwe

Rais wa Ukraine aliyeondolewa madarakani Victor Yanukovych amefunguliwa mashtaka
Ukraine imetoa hati ya kukamatwa kwa Rais aliyeondolewa madarakani, Victor Yanukovych, Waziri wa mambo ya ndani wa mpito ametangaza hatua hiyo.
Arsen Avakov amesema katika ukurasa wa Facebook amesema kesi dhidi yake imefunguliwa dhidi ya Yanukovych na maafisa wengine kuhusu mauaji ya makubwa ya watu.
Wabunge walipiga kura kumuondoa Yanukovych siku ya jumamosi baada ya maandamano ya miezi kadhaa yaliyojitokeza baada ya kupinga kujiunga na Umoja wa Ulaya.
Machafuko yaliyotokana na maandamano hayo yalisababisha watu kadhaa kupoteza maisha juma lililopita.
Avakov amesema Yanukovych alionekana mjini Balaklava siku ya jumapili, lakini mpaka sasa hajulikani mahali alipo.
BBC

No comments: