Saturday 13 December 2014

Roy Keane adaiwa alizua migogoro Villa

 

Aliyekuwa naibu mkufunzi wa kilabu ya Aston Villa Roy Keane
  
Naibu Kocha wa Kilabu ya Aston Villa Roy Keane na mshambuliaji Gabriel Agbonlahor nusra wapigane wakati wa mazoezi katika majibizano ya manane yaliomlazimu kocha huyo kuondoka katika kilabu hiyo.
Kulingana na gazeti la Daily mail nchini Uingereza,Roy Keane mara kwa mara alihusika katika mgogoro na wachezaji wa muhimu wa kilabu hiyo miezi sita tu baada ya kujiunga na kilabu hiyo.
Inadaiwa kuwa hali ya mazingira wakati wa mazoezi ilibadilika mara kwa mara wakati wa kuwasili kwa Roy Keane.
Kulikuwa na hali ya wasiwasi wakati kocha huyo alipozozana na nahodha wa kilabu hiyo Agbonlahor mbele ya wachezaji wenzake wakati wa mazoezi kabla ya naibu huyo kuondoka katika timu hiyo.


                      Nahodha wa kilabu ya Aston Villa Agbonlahor akielekea kufunga bao

Inadaiwa kuwa Agbonlahor alikuwa akijadiliana na mkufunzi wa timu hiyo Lambert wakati Keane alipoingilia kati.
Lakini Agbonlahor alikataa kunyamaza na badala yake akamwambia Keane kwamba anazungumza na kocha.
Wawili hao baadaye walihusika katika majibizano na ilibidi watawanywe.
Uhasama huo uliendelea kati ya wawili hao ndiposa Lambert akafanya kikao na Roy Keane wakati ilipoamuliwa kwamba nahodha huyo wa kitambo wa timu ya Manchester United ataondoka katika kilabu hiyo

No comments: