Saturday 13 December 2014

Mayweather kuchapana na Pacquiao Mei 2


Mayweather akipigana.Bondia huyo amesema kuwa yuko tayari kutetea taji lkake dhidi ya Manny Pacquiao mwaka ujao. 


Bondia Floyd Mayweather ametaja tarehe 2 mwezi May mwaka 2015 kama siku ya pigano kati yake na Manny Pacquiao .
Kulingana na gazeti la Daily mail nchini Uingereza ,uvumi kwamba pigano hilo ambalo litakuwa la kiwango kikubwa cha malipo kuwahi kutokea katika historia ya ndondi ulianza pale Pacquiao alipoonyesha mchezo mzuri kati yake na Chris Algieri mjini Macau wiki mbili zilizopita.
Na sasa Maywheather kupitia kampuni yake moja ya mauzo amesema kuwa yuko tayari kupambana na Pacman katika pigano lake linalokuja.
 

Bondia Manny Pacquiao Kushoto akimchapa Tim Bradley katika mojwapo ya mapigano yao.
Bondia huyo ambaye ndiye mwanamichezo tajiri duniani amesema kuwa mashabiki wa ndondi wamesubiri sana pigano hilo na sasa yuko tayari.
''Kizuizi kikubwa cha pigano hilo ni promota wa Pacquiao Bob Arum ,lakini najua kwamba sisi sote tunalihitaji pigano hili'',alisema Mayweather.. Kwa hivyo ni wakati lifanyike.
Mayweather alikiri kwa mara ya kwanza majadiliano yanaendelea kwa siri na kuongeza kwamba hamuogopi mtu yeyote.''Miaka iliopita tulikuwa na tatizo la kupimwa mikojo na damu,swala ambalo Pacman amekuwa akilipinga''.aliongezea Mayweather.

 

Bondia Mayweather baada ya kushinda katika baadhi ya mapigano yake.
Hatahivyo upande wa Mayweather ni vile kitita cha pigano hilo kitakavyogawanywa.
Inakadiriwa kuwa pigano hilo litagharimu dola millioni 300.
Upande wa Pacman tayari umekubali fedha hizo kugawanywa kwa 60-40 huku Mayweather akichukua kitita kikubwa,ijapokuwa kuna madai kwamba Mayweather huenda akadai asilimia kubwa zaidi iwapo makubaliano yataafikiwa

No comments: