Monday 8 December 2014

Alichokisema msichana aliyemtesa mtoto Uganda leo na maamuzi yaliyotolewa na Mahakama

NYUND
Unamkumbuka yule mfanyakazi wa ndani aliyemtesa mtoto nchini Uganda na kuteka hisia za watu wengi duniani? leo kesi yake imeweza kusomwa kwa mara nyingine.
Mfanyakazi huyo Jolly Tumuhirwe mwenye miaka 22 aliiambia mahakama nchini humo leo kuwa anajua kile alichokifanya na anakiri kosa hivyo anaomba watu wamsamehe kwa kuwa alifanya makosa.
Mfanyakazi huyo wa nyumbani aliyenaswa kwenye kanda ya video akimpiga mtoto wa bosi wake ajulikanaye kwa jina la Arnella mwenye umri wa miezi 18 pia alikua akimkanyaga mtoto huyo bila huruma.
kipig
Licha ya taarifa ya polisi kusema Jolly atashitakiwa kwa kosa la jaribio la mauaji, kiongozi wa mashitaka alimshitaki kwa kosa la kumtesa mtoto mdogo.
Msichana huyo alikiri makosa yake na kuomba msamaha na Hakuna wakili yeyote aliyemwakilisha Jolly mahakamani hapo licha ya mmoja wa mawakili mashuhuri kusema angemwakilisha Jolly bila malipo ypyote.
Kesi hiyo imeahirishwa tena hadi keshokutwa wakati hakimu akitarajiwa kutoa hukumu dhidi yake.
Binti huyo huenda akafungwa jela miaka 15 au kutozwa faini ya dola za kimarekani 800 au adhabu zote mbili.

No comments: