Saturday 13 December 2014

Mkutano wa mazingira wa UN warefushwa

 Waziri wa mazingira wa Peru akihutubia mkutano mjini Lima 
Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu mazingira ambao ulikuwa umalizike mapema, unaendelea nchini Peru kwa siku ya 13 huku wajumbe wakijaribu kufikia makubaliano kuhusu namna ya kupambana na kuzidi kwa joto duniani.

Wamekwama katika hoja kuhusu ahadi ambazo zinaweza kutolewa na nchi zilizoendelea na zinazoendelea.
Mataifa yanayoharibu mazingira zaidi, kama Marekani na ya Umoja wa Ulaya, yanataka kutangaza mwaka ujao yatapunguza gesi inayozidisha joto kwa kiasi gani.
Lakini piya yanataka nchi nyengine zaidi zitoe ahadi kama hiyo.
Nchi kuu zinazoendelea, pamoja na India na Uchina, zinapinga hayo huku nchi maskini zaidi zinataka msaada zaidi wa fedha ili kupambana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa.

No comments: