Friday 28 November 2014

migogoro ndani ya Bunge la Afrika Mashariki na kilichoamuliwa

Margaret-Zziwa 
Spika wa Bunge la Afrika Mashariki EALA, Margaret Zziwa amesimamishwa kazi na Wabunge wa Bunge hilo kwa kile kinachoelezwa kuwa amekuwa akiendeleza ubaguzi kwenye ajira, ufisadi na pia hana uongozi bora.
Katika mahojiano aliyoyafanya na kituo cha BBC amekana madai hayo na kusema malumbano yanayoendelea ndani ya Bunge hilo yanatokana na siasa za chuki baina ya Wabunge na kusababisha Bunge hilo kutimiza majukumu yake.
Uchunguzi unafanyika ili kujua kama madai yaliyopelekea kumsimamisha yalikuwa na ukweli wowote.

No comments: