Friday 10 October 2014

MWALIMU AZICHAPA NA MWANAFUNZI WAKE LIVE DARASANI KISA BANGI

Mwalimu wa sayansi katika shule ya Santa Monica High School alimstukia mwanafunzi huyu akijaribu kuuzia wanafunzi wenzake bangi darasani. 

Alipomkabili kuhusu tendo hilo, mwanafunzi huyo alimsukuma mwalimu huyo na ghafla ngumi zikaanza kurushwa hewani.



Mwanafunzi huyo, Blair Moore, alikamatwa na polisi na kufunguliwa mashitaka ya kuingiza madawa, na kisu shuleni.

blair moore Mwalimu na mwanafunzi wapigana darasani. Wanafunzi warekodi video badala ya kuamulia
Mwanafunzi huyo, Blair Moore, akiwa chini ya ulinzi wa polisi
Mwalimu huyo, Mark Black, ambaye pia ni kocha wa mieleka shuleni hapo, alisimamishwa pamoja na malipo kwa muda wakati uchunguzi wa tukio unaendelea; si kama adhabu, bali ni utaratibu wa shule za jimbo hilo.



Wanafunzi wengi walijitokeza kum-support mwalimu huyo, kwa kusema alijihami baada ya kushambuliwa kwanza. Walianzisha mpaka Facebook Page, “We Support Coach Black of Samohi” ambayo imepata zaidi ya Likes 20,000. “Samohi” ni kifupi cha Santa Monica High [school]




Mwalimu huyo aliruhusiwa kurudi kazini baada ya uchunguzi kuonyesha hakuwa na hatia
coach black Mwalimu na mwanafunzi wapigana darasani. Wanafunzi warekodi video badala ya kuamulia

Wanafunzi wengi walikuwa upande wa mwalimu huyo

No comments: