Sunday 6 July 2014

SIMU ZA MKONONI ZAWASAIDIA WAGONJWA WA KISUKARI SENEGAL

simu

Kwa mara ya kwanza wagonjwa wa kisukari nchini Senegal wameanza kupokea ujumbe wa simu ukiwataka kufunga kwa kipindi cha kabla, wakati na baada ya mwezi wa Ramadhan.
Senegal imekuwa nchi ya kwanza kuanza kutumia huduma hiyo ya simu kuwasaidia wagonjwa kisukari njia muhimu na salama za kuweza kukabiliana na kulinda afya zao haswa katika kipindi hiki cha mfungo.
Wagonjwa walioanza kupokea huduma hiyo wanasema inawasaidia sana.
Marie Gadio, mwenye umri wa miaka 26, ambaye aligundulika kuugua ugonjwa wa kisukari akiwa na miaka 13 anasema kuwa kukabiliana na ugonjwa huo kipindi cha mwezi wa Ramadhan sio kitu rahisi

No comments: