Wednesday 5 March 2014

NYOKA WANAVYOGEUZWA KUWA MIKOBA ILI UPENDEZE


Je unatumia bidhaa kama mikanda, mabegi, viatu na wakati mwingine nguo zinazotumia ngozi ya nyoka, leo nakuletea picha hapa uone jinsi nyoka wanavyouawa na kuchunwa ngozi ili wewe upendeze.

Kuna njia mbalimbali zinazotumika kuua na kuchuna ngozi ya nyoka huko Indonesia. Lakini njia ambayo ni ukatili ambapo nyoka wanauawa na kuchunwa ngozi kwaajili ya kutengeneza mikoba haswa na kuuzwa nchi za Magharibi kwa zaidi ya shilingi milioni 6.5 (pauni za Uingereza 2400).
Pamoja na gharama yote hiyo huko Ulaya na Marekani, mkoba huo unapatikana kwa sawa na shilingi za Kitanzania 54,000(pauni 20) nchini Indonesia kwenye soko la ngozi ya nyoka ambapo nguo na vipuri mbalimbali huuzwa.
Moja ya machinjio ya nyoka yalionesha jinsi nyoka wanavyovuliwa ngozi yao ni kijiji kimoja kijulikanacho kama Cirebon, nchini Indonesia. Ukiangalia katika picha hizi utaona jinsi wafanyakazi wanavyoua na kuchuna ngozi nyoka zaidi ya elfu kwa wiki.
Katika maeneo hayo bei ya mkoba uliotengenezwa kwa ngozi ya nyoka unaweza kuwa kati ya shilingi 24,000(pauni9) mpaka 48,000 kutegemea na ukubwa. Ngozi ya nyoka inapofika nchi za Magharibi katika nyumba za mitindo bei hupanda maradufu mpaka awa na shilingi milioni 6.5
ANGALIA ZAIDI...










No comments: