Thursday 5 June 2014

Avaa kama Rambo na kufanya mauaji ya maafisa watatu wa polisi.

rambo

Wahalifu kila siku wanakuja na mbinu mpya ambapo Polisi nchini Canada wanamsaka mtu hatari mwenye silaha ambaye amevaa mavazi kama ya muigizaji wa filamu za mapigano Rambo. Mtu huyo amewaua kwa kuwapiga risasi maafisa watatu wa polisi na kujeruhi wengine wawili katika tukio hilo la pamoja.
Mashambulizi hayo ya risasi yamefanyika wakati polisi walilipokea simu juu ya mtu aliyekuwa na silaha Kaskazini mwa mji wa Moncton katika Jimbo la Pwani ya Mashariki ya New Brunswick.
rambo2

Maafisa hao watatu waliokwenda katika eneo hilo waliuwawa na wengine kupata majeraha lakini sasa wapo katika hali nzuri.
Mtuhumiwa huyo mwenye umri wa miaka 24 Justin Bourque, kutoka mjini Moncton, anadaiwa kuwa alibeba silaha nzito za mapigano pamoja na visu.
rambo3

Polisi waliweka picha ya mwanaume huyo akiwa amevaa mavazi ya kijeshi na kushika bunduk

No comments: